• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wizara ya Madini watatua mgogoro baina ya wananchi na mwekezaji

Posted on: November 11th, 2022

Wizara ya Madini leo tarehe 10 Novemba, 2022 imeitisha kikao cha wadau muhimu kujadili mgogoro wa baina ya Mgodi wa Cata Mining Limited uliopo katika Wilaya ya Butiama na jamii inayouzunguka mgodi huo baada ya kupokea malalamiko mbalimbali kuhusu mgodi huo na mahusiano yake na jamii.  

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa ameutaka mgodi wa Cata Mining Limited kuwalipa wananchi waliotoa maeneo yao kupisha uwekezaji wa mgodi katika eneo hilo.

Aidha, Mheshimiwa Dkt. Kiruswa ameutaka mgodi huo kuchangia huduma za jamii kwa mujibu wa sheria za madini kwa maedeleo ya wananchi wanaouzunguka mgodi huo.

“Suala la kuchangia huduma za jamii inayozunguka mgodi ni suala la kisheria sio hisani wala msaada na linapaswa kuzingatiwa kila wakati” alisema Mheshimiwa Kiruswa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee ameishukuru Wizara kwa kupokea malalamiko ya wananchi hao na kuitisha kikao hicho ambacho kimehudhuriwa na wadau wote muhimu katika utatuzi wa mgogoro huo.

Mheshimiwa Mzee ameahidi kuwa Ofisi yake itafuatilia kwa karibu utekelezaji wa maagizo yote ya Serikali na kuhakikisha wananchi wanaouzunguka mgodi huo wanapata stahiki yao kutoka kwa mwekezaji anayemiliki lesseni ya uchimbaji katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Kaimu Kamishna wa Madini Bwana Msechu Mwaluvoko ameeleza kuwa katika mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017, kifungu namba 105 kinachomtaka mmiliki wa lesseni za madini kuchangia huduma kwa jamii inayozunguka mgodi wa madini.  

Bwana Mwaluvoko ameeleza kuwa upo mwongozo wa kuchangia huduma kwa jamii inayouzunguka mgodi ambao unamtaka mwekezaji kuandaa mpango wa kuchangia huduma kwa jamii na kuuwasilisha Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa ajili ya mapitio kabla ya kuanza utekelezaji.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Dkt. Adolf Ndunguru, Naibu Katibu Mkuu Msafiri Mbibo, Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mheshimiwa Moses Kaegele, Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama Bi. Patricia Kabaka.  

Chanzo: Wizara ya Madini

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa