• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wekezeni kwenye miradi ya maendeleo

Posted on: June 15th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kigoma Ali Malima amewataka viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kutumia fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Juni 2020 wakati alipohudhuria kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja mbalimbali zilizotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Badala ya kupeleka asilimia 40 ya makusanyo ya ndani kwenye miradi ya maendeleo kama mnayotakiwa kisheria, mmepeleka asilimia 6.3 tu kwenye miradi ya maendeleo, hii haikubaliki” alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa kutokupeleka fedha kwenye miradi ya maendeleo kama inavyotakiwa ni kuwaonea wananchi wa halmashauri hiyo na waathirika wakuu ni madiwani ambao watarudi kwa wananchi kwenda kuomba kura.

Mheshimiwa Malima amewataka madiwani kuwasimamia watendaji ili wapeleke miradi ya maendeleo inayohitajika kwa wananchi waliowachagua.

Aidha Mheshimiwa Malima ameipongeza halmashauri hiyo kwa kufanya vizuri katika ukaguzi wa CAG kwa mwaka 2018/2019 ambapo pamoja na kupata hati safi pia walikuwa na hoja 13 mpya wakati hoja 31 zilikuwa za miaka ya nyuma.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kutoa maelezo ya makubaliano kati ya halmashauri hiyo na SUMA JKT kuhusu fedha ambazo halmashauri hiyo inadai kwa SUMA JKT ifikapo tarehe 30 Juni 2020.

Mkuu wa Mkoa pia ameitaka halmashauri hiyo kuwasilisha mpango wa kulipa madeni mbalimbali ya halmashauri hiyo na ukomo wa kulipa madeni hayo kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara.

“Mnatakiwa kumpa maelezo ya kina Katibu Tawala hili deni la bilioni 1.2 litalipwaje na kwa muda gani litalipwa” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha Mheshimiwa Malima aliitaka halmashauri hiyo kuimarisha mapato yatokanayo na uvuvi na kilimo cha mazao ya chakula na biashara ili kuweza kuongeza mapato ya ndani ya halmashauri hiyo.

Wakati huo huo madiwani walitumia fursa hiyo kuomba Mkuu wa Mkoa aweze kuwasaidia katika changamoto mbalimbali zinazowakabili katika kata zao.

Changamoto zilizotajwa ni pamoja na ubovu wa barabara kwa sababu barabara nyingi za halmashauri hiyo hazipitiki wakati wa mvua; kutokupatikana mawasiliano ya simu katika kata na vijiji vilivyopo katika mpaka wa Tanzania na Kenya; maombi ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Nyamagaro ambacho kimeanza kujengwa kwa nguvu za wananchi.

 Changamoto nyingine ni matatizo ya umeme wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA) ambapo madiwani walilalamikia baadhi ya taasisi na vitongoji kutokuunganishiwa umeme; maombi ya ujenzi wa madaraja; na maombi ya sekondari ya kidato cha tano na sita katika tarafa ya Nyacha.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa