• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wekeni mpango wa matumizi bora ya ardhi-Mtambi

Posted on: May 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe.Kanali  Evance Alfred Mtambi leo amezungumza na wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kuitaka Halmashauri hiyo kuanzisha mpango wa matumizi bora ya ardhi.

“Mkoa wa Mara tunalo tatizo kubwa la migogoro ya ardhi linalotokana na ongezeko la idadi ya watu huku eneo likibakia kuwa ni lile lile” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amesema Mkoa wa Mara una Kilomita za mraba 30,130 na asilimia 36 ya eneo lote ni Ziwa Victoria na mito, asilimia 36.6 ni Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mapori ya Akiba na maeneo ya Wildlife Management Area (WMA)  na asilimia 27.4 tu ya eneo lote ni eneo la kilimo, makazi, ufugaji, ujenzi, taasisi, viwanda, uchimbaji wa madini na kadhalika.

Kanali Mtambi amesema kwa Sensa ya Watu na MAkazi, Mkoa una watu zaidi ya milioni 2.5 wanaongezeka kwa wastani wa asilimia 3.1 kwa mwaka jambo ambalo lisipopangiliwa litaongeza zaidi migogoro ya kugombea ardhi.

Mhe. Mtambi ameeleza kuwa kwa sasa asilimia kubwa ya wananchi wanaokuja ofisini kwake wanamgogo wa ardhi na kuitaka Halmashauri ijipange kuweka matumizi bora ya ardhi ili kupata maeneo ya malisho, mashamba ya kilimo, vyanzo vya maji na kadhalika ili kupunguza migogoro.

Mhe. Mtambi ameeleza kuwa kwa sasa kutokana na kuwepo kwa wawekezaji baadhi ya vijiji vimeanza kugombea mipaka ya vijiji na baadhi ya vijiji kuendelea kuomba Hifadhi ya Taifa ya Serengeti isogezwe jambo ambalo linaharatisha uchumi wa Taifa na taswira ya nchi katika jumuiya ya kimataifa wananchi wanapozidi kuisogelea Hifadhi.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka Walimu na Wakuu na Wakuu wa Shule kudhibiti maadili ya wanafunzi na watumishi mashuleni na kuwafundisha wanafunzi kwa kuzingatia weledi.

Mhe. Mtambi pia amewataka watumishi kuwahamasisha wananchi kubadilisha mfumo wa maisha na kufuga kisasa, kutumia nishati safi katika kupika na kuepuka matumizi ya kuni na mkaa.

Amewataka watumishi kusimamia miradi ya maendeleo kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na maelekezo ya Serikali katika mradi husika na kumtaka Mkuu wa Wilaya kufuatilia Kituo cha Afya Machochwe na ujenzi unaoendelea katika Hospitali ya Wilaya ya Serengeti.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Vincent Mashinji akizungumza katika kikao hicho ameeleza kuwa kwa sasa Wilaya ya Serengeti inatekeleza mradi mkubwa wa umeme wenye thamani ya shilingi bilioni 4.6  na mradi wa maji wa shilingi bilioni 21 katika Mji wa Mugumu.

Aidha, Mhe. Mashinji ameeleza kuwa Halmashauri imeendelea kulipa deni la watumishi wa Halmashauri hiyo shilingi milioni  500 kulingana na upatikanaji wa fedha na kwa sasa Halmashauri imedhibiti uhamishaji wa kiholela kw awatumishi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa