• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waziri wa Maji afanya ziara Mkoa wa Mara

Posted on: October 10th, 2022

Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso leo tarehe 8 Oktoba, 2022 amefanya ziara ya siku moja katika Mkoa wa Mara ambapo amezindua Bodi ya Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA), ametembelea mradi wa maji wa Kitende na kukabidhi mradi wa maji wa Rorya- Tarime kwa mkandarasi.

Akiwa katika Wilaya ya Musoma, Mheshimiwa Aweso amezindua Bodi ya tisa ya MUWASA na kuipongeza Bodi hiyo pamoja na Menejimenti kwa kazi nzuri wanaoifanya kuboresha huduma za maji katika Manispaa ya Musoma.

Mheshimiwa Aweso amezitaka Mamlaka za maji hapa nchini kuja kujifunza MUWASA na namna ya kupandisha utendaji na molali ya wafanyakazi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akiwa katika Wilaya ya Rorya, Mheshimiwa Aweso ametembelea ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Rorya na kupokelewa na Mwenyekiti wa Wilaya pamoja na viongozi wengine.

Baadaye ametembelea mradi wa maji wa katika Kata ya Ktembe uliochimbwa na mdau wa maendeleo Bwana Joseph Obeyo na baadaye kukabidhi kisima hicho kwa Serikali ili iweze kusambaza maji kwa wananchi.

Akiwa katika mradi huo, Mheshimiwa Aweso ameahidi kutoa shilingi 400,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa tenki na mtandao wa usambazaji wa maji katika eneo hilo.

Mheshimiwa Aweso pia alitembelea Kijiji cha Nyang’ombe katika Kata ya Nyamigaro ambapo alikabidhi mradi wa shilingi bilioni 134 kwa mkandarasi na kumtaka mkandarasi huyo kufanya kazi kwa ubora na haraka kukamilisha mradi huo kwa mujibu wa mkataba.

“Mimi niwahakikishie wananchi kuwa Wizara ya Maji haitacheka na mkandarasi, itacheka na maji” alisema Mheshimiwa Aweso.

Aidha, Mheshimiwa Aweso amewaahidi wananchi wa kata 10 za Wilaya ya Rorya na kata 8 za Wilaya ya Tarime kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 30 kuanzia sasa na baada ya hapo wategemee kupata maji safi na salama ya uhakika.

Mheshimiwa Aweso amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa mkandarasi na wataalamu wanaosimamia mradi huo ili ukamilike kwa haraka waweze kupata maji kwa haraka zaidi.

Akizungumza katika maeneo mbalimbali, Mbunge wa Rorya Mheshimiwa Jafari Chege amemshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kukamilisha miradi yam aji iliyokuwa imekwama kwa muda mrefu katika Wilaya ya Rorya.

Aidha Mheshimiwa Chege amemuomba Waziri kuruhusu mradi unavyoendelea kujengwa, wananchi wanaoishi karibu na chanzo cha maji kuanza kupata maji kabla mradi mzima haujakamilika.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Waziri aliambatana na Wakuu wa Wilaya za Musoma, Tarime na Rorya, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, viongozi na menejimenti ya MUWASA, Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) pamoja na baadhi ya mameneja wa mamlaka za maji za Kanda ya Ziwa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa