• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waziri wa Madini apiga marufuku uchimbaji usiku

Posted on: June 15th, 2020

Waziri wa Madini Mheshimiwa Dotto Biteko amepiga marufuku uchimbaji wa madini usiku kwa wachimbaji wadogo katika Mgodi wa Irasanilo uliopo katika eneo la Buhemba katika Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Biteko ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Juni 2020 wakati alipokuwa anazungumza na wachimbaji na wananchi wa eneo la Buhemba kufuatia ajali iliyotokea katika eneo hilo na kuua wachimbaji wawili na wengine nane kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo.

“Kuanzia sasa shughuli zote za uchimbaji katika eneo hili zifanyike mchana ni marufuku kufanyika usiku” alisema Biteko. Aidha amemtaka mwajiri wa wachimbaji waliofariki na waliojeruhiwa katika ajali hiyo kulipa fidia, kugharamia matibabu, mazishi na msiba kwa mujibu wa sheria.  

Mheshimiwa Biteko aliwataka wananchi na viongozi wa mgodi huo kuheshimu sheria za nchi na kuzifuata na kupunguza migogoro isiyokuwa na tija baina ya wachimbaji na viongozi wa mgodi.

Aidha ameutaka mgodi huo kuchangia katika miradi ya maendeleo katika vijiji vinavyowazunguka kwa mujibu wa sheria. “Kuanzia kesho mgodi huu uanze kulipa mrahaba kwa mujibu wa sheria ili vijiji navyo viweze kupata chochote kutokana na uwepo wa mgodi hapa”. Alisema Biteko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa serikali ya Mkoa wa Mara imejipanga vizuri katika kushughulikia watu wote wanaofanya ubabe katika mgodi huo.

“Nimeambiwa katika mgodi huu kuna wababe hapa ambao wanajifanya kuwa wao ndio serikali sasa sisi katika Mkoa wa Mara tumejipanga vizuri, tutawanyoosha” alisema Malima.

Mheshimiwa amewataka wachimbaji hao kuchimba madini na kutafuta riziki yao vizuri kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.  

“Mimi ninatamani pawepo na uongozi unaoeleweka na kuheshimiwa na wote ili hata sisi wengine tuusikilize huo na sio kila mtu anakuwa kiongozi katika eneo hili” alisema Malima.

Mgodi wa Isaranilo unamilikiwa na wachimbaji wadogo wadogo na tayari una lesseni 15 ambazo zinatambulika kisheria lakini kwa siku za hivi karibuni umekumbwa na migogoro baina ya wachimbaji na wasimamizi wa mgodi huo.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa