• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waziri Mkuu aiagiza TAKUKURU kuchunguza Wizi Butiama

Posted on: February 28th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.) leo ameiagiza Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuwafuatilia na kuwachukulia hatua watumishi wa Wilaya ya Butiama waliohusika na matumizi ya fedha za Serikali kinyume na utaratibu.

Akizungumza na watumishi na viongozi wa Wilaya ya Butiama katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Mhe. Majaliwa amesema katika wizi huo viongozi wa OR-TAMISEMI, Baraza la Madiwani na viongozi wengine wa Wilaya ya Butiama hawakuweza kuubaini.

“Tarehe 13 Juni, 2022 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama aliandika barua kwenda Hazina kuwajulisha kuwa kutakuwa na fedha za ziada shilingi 736,228,732 ambazo wanaomba kibali wazihamishe na kabla ya kupata kibali aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo akahamisha shilingi milioni 886, shilingi milioni 150 iliongezwa na wahasibu kwa kutumia vibali walivyokuwa navyo “amesema Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema Julai, 2022 Halmashauri ilituma shilingi 306 lakini baadaye wakarudisha Hazina shilingi milioni 98 zikabakia milioni 208 bila kulijulisha Baraza la Madiwani, wakuu wa Idara na Vitengo vingine kuhusu kuwepo kwa fedha hizo na baadaye shilingi milioni 151 zilitumika katika maeneo ambayo tayari Halmashauri ilikuwa na bajeti.

“Fedha hizo zilitumika kwenye TASAF, Sensa ya Watu na Makazi, AMREF, kupanga na kupima ardhi, marejesho ya mishahara na shilingi milioni 12 ununuzi wa vifaa vya nyumba ya Mkurugenzi” amesema Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema haya matumizi yote yalikuwa ni njia ya kutolea fedha hiyo na ndio maana orodha yake haikupelekwa kwenye Baraza la Madiwani.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Butiama alipoulizwa na Timu iliyoundwa na Ofisi ya Waziri Mkuu alisema hakuwa na taarifa ya uwepo wa fedha hizo na shilingi milioni 57 ambazo bado zilikuwepo katika akaunti zilizuiwa nab ado zipo.

 Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama cha Mapinduzi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa