• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wavuvi wasalimisha zana haramu za uvuvi baada ya kupewa elimu Musoma

Posted on: June 26th, 2021

Wavuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma wamesalimisha zana haramu za uvuvi 1,407 zenye thamani ya shilingi 162,630,0000 baada ya kuelimishwa kuhusu madhara ya kutumia zana hizo.

Hayo yameelezwa leo tarehe 25 Juni 2021 na Kaimu Afisa Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Bwana Mbuni Oyondi wakati akisoma taarifa ya zana haramu zilizokuwa zinahitaji kuteketezwa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa.

“Nyavu hizi zimesalimishwa na wananchi kwa hiari baada ya kupatiwa elimu ya mara kwa mara kutoka kwa wataalamu wa uvuvi kwa kushirikiana na vikundi vya ulinzi shirikishi wa rasilimali za uvuvi” ameeleza Bwana Oyondi.  

Kwa mujibu wa Bwana Oyondi, kati ya zana haramu zilizosalimishwa  makokoro ya sangara ni 55, nyavu za plastiki (timba) ni 1,330 na nyavu ndogo chini ya nchi sita 22.

Bwana Oyundi ameeleza kuwa Halmashauri hiyo inawahamasisha wavuvi kujiunga kwenye vikundi vya ushirika ili kuwa na uvuvi endelevu.

“Tangu Januari 2021 hadi Mei 2021 vikundi 21 vya wavuvi vimepatiwa elimu ya ushirika na tayari vikundi vinne vya ushirika vya wavuvi vimesajiriwa, vikundi vitatu vipo katika hatua za awali za usajiri” ameeleza Bwana Oyundi.

 Kwa mujibu wa Bwana Oyundi Halmashauri inategemea kuwa ushirika wa wavuvi utakuwa chachu ya kulinda na kuendeleza rasilimali za uvuvi.

Ameeleza kuwa katika Mwaka wa fedha 2019/2020 sekta ya uvuvi iliingiza shilingi 849,730,384 ambayo ni sawa na asilimia 60 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.  

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ina jumla ya wavuvi 8,263 wanaovua katika vijiji 40 vinavyozunguka Ziwa Victoria.

Akizungumza wakati wa kuteketeza nyavu hizo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Lt. Josephine Paul Mwambashi amewapongeza sana wavuvi kwa kusalimisha zana haramu kwa hiari.

“Ninaomba niwapongeze sana kwa uamuzi wenu wa kusalimisha zana haramu za uvuvi, kitendo hiki ni kikubwa na kinahitaji kuigwa na wavuvi wengine hapa nchini” amesema Bibi Mwambashi.

Mwenge wa uhuru ukiwa katika Wilaya ya Musoma umeweka jiwe la msingi katika zahanati ya Kamunyonge; umeweka jiwe la msingi katika bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Mwisenge; na umetembelea mfumo wa Benki Kuu wa usajiri wa vikundi vya huduma ndogo ya fedha.

Aidha Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika mradi wa maji wa Etaro; umeweka jiwe la msingi jengo la utawala katika Sekondari ya Kigera Etuma; na kuteketeza zana za uvuvi haramu na kupanda miti katika Sekondari ya Kigera Ituma.

Baada ya hapo Mwenge wa Uhuru umetembelea mradi wa kitalu nyumba na kuweka jiwe la msingi katika karakana za ufundi katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDPC) Musoma; na kutembelea kiwanda kidogo cha kutengeneza sabuni cha wanawake na kiwanda cha kutengeneza viatu cha vijana.

Aidha mkesha wa Mwenge unaendelea katika Shule ya Msingi Nyakato iliyopo katika Manispaa ya Musoma na kesho utakabidhiwa katika Wilaya ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa