• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watumishi wakumbushwa kutimiza wajibu wao

Posted on: April 8th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bwana Msalika Robert Makungu leo amekabidhi Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kwa Bwana Bwana Gerald Musabila Kusaya katika ukumbi wa uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo, Bwana Kusaya amewataka watendaji wa Serikali Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wananchi na kutoa ushirikiano baina yao na kwa viongozi katika utendaji kazi.

“Kila mtu kwenye nafasi yake akitimiza wajibu wake, kazi yangu itakuwa rahisi sana na kama kuna jambo limeshindikana, mimi nipo na kwa pamoja tunaweza kulitatua au kutafuta suluhisho kwa viongozi wengine wa Serikali” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amesema heshima ambayo watendaji wa umma wanaipata inatokana na nafasi waliyoipata na kuongeza kuwa vyeo ni dhamana na inahitaji kutimiza majukumu ili kuendelea kukitendea haki na kukiheshimisha cheo kilichopo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara pia amewataka wasimamizi wa kazi kwa nafasi mbalimbali za utumishi wa umma kuwasimamia watumishi waliochini yao na kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha, Bwana Kusaya amemshukuru Rais kwa kuendelea kumuamini na kuwashukuru viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Mara kwa mapokezi mazuri aliyoyapata tangu alipowasili kwa ajili ya kuanza kazi katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bwana Msalika Robert Makungu amewashukuru watumishi wa Mkoa wa Mara kwa ushirikiano waliompa tangu alipoanza kutekeleza majukumu yake mwezi Agosti, 2022 hadi allipohamaishwa.

Bwana Makungu amewataka watumishi kumpa ushirikiano Katibu Tawala mpya ili umsaidie kuwahudumia vizuri wananchi wa Mkoa wa Mara.

Bwana Makungu ameongelea umuhimu wa kuimarisha menejimenti za Halmashauri (CMT) ili ziweze kushauri Mabaraza ya Madiwani kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi katika masuala mbalimbali.

Bwana Makungu ametumia fursa hiyo kuwakaribisha watumishi kuwekeza katika kilimo na ufugaji katika  Mkoa wa Rukwa.

 Hafla ya makabidhiano imehudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala Wasaidizi na Wakuu wa Vitengo, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na  watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa