• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watumishi waaswa utunzaji nyaraka za miradi

Posted on: June 24th, 2021

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Lt. Josephine Paul Mwambashi amewaasa watumishi wa Umma wanaohusika katika kusimamia miradi ya umma kuhakikisha wanatunza nyaraka na vielelezo vyote vya miradi hususan inayohusu matumizi ya fedha.

Kauli hiyo imetolewa kwa nyakati tofauti leo tarehe 24 Juni 2021 wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru zilizofanyika katika wilaya ya Rorya.

“Wataalamu hakikisheni mnatunza vizuri nyaraka zote za miradi ili hata zinapokuja kukaguliwa kusiwe na maswali mengi kuhusiana na utekelezaji wa mradi” ameeleza Mwambashi.

Amempongeza Mkuu wa Shule Sekondari ya Nyathorogo Mwalimu George Thobias Minanago kwa utunzaji mzuri wa nyaraka na vielelezo mbalimbali vinavyohusiana na ujenzi wa mradi wa vyumba viwili vya madarasa.

“Mara nyingi tunaamini wanawake ndio wasimamizi wazuri wa miradi lakini leo  mwalimu ametuonyesha kuwa hata wanaume wanaweza kusimamia miradi vizuri na kutunza nyaraka vizuri, ninakupongeza sana” alisema Mwambashi  

Aidha amepongeza pia uhifadhi wa nyaraka katika Kituo cha Afya Utegi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ambacho Mwenge wa Uhuru umekizindua leo.

Mwenge wa Uhuru leo umetembelea kiwanda cha viatu vya ngozi cha Credo Leather Industry; mradi wa barabara ya Tingirime hadi Nyanchabakenye;  na baadaye ukazindua kiwanda cha mafuta ya kupikia ya alizeti cha Nyihita Sunflower Cooking Oil Production kilichopo katika eneo hilo hilo la Nyanchabakenye.

Baada ya hapo mwenge uliweka jiwe la msingi katika Shule ya Sekondari  ya Kuruya na kuzindua madarasa mawili yaliyojengwa na Serikali na kukagua klabu ya kupambana na kuzuia rushwa katika Shule ya Sekondari ya Nyanthorogo .

Aidha Mwenge wa Uhuru umetembelea Shule ya Msingi Utegi kuangalia utunzaji wa mazingira na wakimbiza mwenge kitaifa walipata wasaa ya kupanda miti ya kumbukumbu katika viwanja vya shule hiyo.  

Wakati huo huo, Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru amekataa kuuzindua mradi wa maji katika shule ya Sekondari ya Buturi kutokana na mapungufu mbalimbali ikiwemo utunzaji wa nyaraka za mradi huo pamoja na utata katika uandishi wa madai ya malipo ambapo watoa huduma hawakutaja aina na kiasi cha bidhaa vilivyokuwa vinanunuliwa.  

Amemuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kudhibiti na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza vielelezo na nyaraka za mradi huo na kutoa taarifa za awali leo jioni.

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Rorya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya pamoja na menejimenti yake kutoa maelezo kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo siku ya Jumatano tarehe 29 Juni 2021 ofisini kwake.

Mbio za Mwenge wa Uhuru katika wilaya ya Rorya zimehitimishwa jioni hii kwa mkesha wa mwenge ambao unafanyika katika mji wa Utegi na kesho unatarajiwa kukabidhiwa katika Wilaya ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa