• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watoto 481,104 kupata chanjo Mara

Posted on: February 15th, 2024

Jumla ya watoto 481,104 wenye umri wa miezi tisa hadi miaka mitano wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya magonjwa ya Surua na Rubella katika Mkoa wa Mara kuanzia leo tarehe  15 Februari, 2024 hadi tarehe 18 Februari, 2024.

Akizindua zoezi la utoaji wa chanjo hiyo katika Kituo cha Afya Nyasho, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda amesema chanjo hiyo ni salama na  muhimu sana kwa watoto na amewapongeza wazazi na walezo na waliojitokeza kuwaleta watoto kupata chanjo.

“Ninawapongeza zaidi akina Baba ambao wamefika hapa kwa ajili ya kuleta watoto kupata chanjo kwa kuonyesha mfano mzuri katika jamii kwa kuzingatia mambo muhimu katika malezi ya watoto, ikiwemo chanjo” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda amewataka wananchi kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kupata chanjo hiyo wanapata na kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu wa afya kuhusu chanjo na masuala ya afya kwa ujumla kwani mtoto asiyepata chanjo zote ni hatari kwa afya yake na afya ya wengine wanaomzunguka.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa kama kauli mbiu inavyosema “onesha upendo mpeleke mtoto akachanje”amewataka wazazi, walezi na jamii kuonyesha upendo wao kwa watoto kwa kuhakikisha wanapata chanjo hii muhimu.  

Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa ngazi za vijiji, Kata, Tarafa na Wilaya kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa Sekta ya Afya ili kuweza kufanikisha zoezi la chanjo katika Mkoa wa Mara.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amewapongeza watumishi wa Kituo cha Afya Nyasho, Manispaa ya Musoma kwa kazi yanayoifanya katika kuhudumia idadi kubwa ya wagonjwa ikilinganishwa na idadi ya watumishi waliopo katika kituo hicho.

Mhe. Mtanda amewataka kuendelea kutoa huduma wakati Serikali inaendelea kukarabati na kuboresha Hospitali ya Manispaa ya Musoma ambayo inatarajiwa kupunguza idadi ya wagonjwa wanaotibiwa katika Kituo cha Afya Nyasho.   

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalfani Haule ameeleza kuwa Wilaya ya Musoma inatarajia kutoa chanjo kwa watoto 86,000 ambapo kati ya watoto hao Manispaa ya Musoma inatarajiwa kuchanja watoto 29,000 na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma inatarajia kuchanja watoto 57, 000.

Dkt. Haule amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuchagua kuzindua chanjo hiyo Kimkoa katika Wilaya ya Musoma na kwa kutenga muda na kushiriki katika uzinduzi huo.

 Uzinduzi huo umehudhuriwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mara Dkt. Zabron Masatu; Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. William Gumbo, mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na  watumishi wa Manispaa ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa