• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wasimamizi wa Elimu wahimizwa kutimiza wajibu

Posted on: December 19th, 2023

Mradi wa Shule Bora kwa kushirikiana na Wakala wa Mandeleo ya Elimu Tanzania (ADEM) wameendesha mafunzo ya siku moja ya wasimamizi wa Elimu katika ngazi mbalimbaliza Mkoa wa Mara na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ikiwa ni kuwajengea uwezo wasimamizi wa elimu kutekeleza majukumu yao.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi na wasimamizi wa shule kwa viongozi wa ngazi za Mkoa na Wilaya ya Serengeti yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Mapinduzi A, katika mji wa mugumu, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo Bwana Ayoub Mbilinyi amewataka wasimamizi hao kutimiza wajibu wao.

Bwana  Mbilinyi amewapongeza mwezeshaji wa mafunzo haya kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuwataka washiriki kuzingatia mafunzo hayo katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku.

Aidha, amewasistiza wasimamizi wa ngazi zote kuwasikiliza walimu na kutatua baadhi ya changamoto zao ili walimu wafundishe wakiwa na amani, na kufanya hivyo hakuhitaji fedha wala rasilimali nyingine ni kuwasikiliza tu. 

 Bwana Mbilinyi ametoa mfano kuwa kuna wakati Mkoa ulikuwa na makambi ya wanafunzi katika masomo mbalimbali na walimu waliokuwa wanafundisha wanafunzi walipewa chakula tu bila posho yoyote na kazi ilifanyika vizuri.

Bwana Mbilinyi amewataka wasimamizi wa elimu walioshiriki mafunzo hayo kuyasambaza kwa maafisa  wengine katika makundi tofauti tofauti ambao hawakubahatika kushiriki mafunzo hayo. 

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Bwana James Johannes amewakaribisha washiriki na kuushukuru Mradi wa Shule Bora na wataalamu wa ADEM kuwapitisha wasimamizi wa elimu katika mafunzo ambayo walimu wakuu wa shule za msingi watafundishwa.

“Hii ni fursa kubwa kwetu kufundishwa angalau kwa juu juu kitu ambacho watu tunaowasimamia watafundishwa kwa muda wa siku tatu, haijawahi kutokea wasimamizi wafundishwe watakachoenda kufundishwa walimu wao, tunashukuru sana” amesema Mwal. Johannes.

 Aidha, Mwalimu Johannes amewataka washiriki kutumia fursa ya mafunzo haya kuongeza uelewa wao katika masuala muhimu ya kwenda kuyasimamia na kuwashukuru wakufunzi kwa kuwaelewesha kuhusu Jumuiya za kujifunza ambazo zitaundwa kwa ajili ya Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa