• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

Posted on: May 29th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mara, Ndugu Gerald Musabila Kusaya leo tarehe 29 Mei, 2025 amefungua kikao cha Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSA) kwa mikoa ya mitatu ya Kanda ya Ziwa na kuwataka walimu kuwaongoza wanafunzi katika kufikia ndoto zao katika maisha.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao hicho, Ndugu Kusaya amesema kuwa walimu ni kiungo muhimu katika maendeleo ya Taifa na kuwaahidi kuwa Serikali ya Awamu Sita itaendelea kuwa begabega na walimu wote hapa nchini Tanzania kutoka shule binafsi na za umma ili kufikia shabaha yake ya kumuinua Mtanzania.

“Muda wote walimu mpo shuleni mnawalea watoto wetu, kikao hiki mkitumie kubadilishana uzoefu wenu hasa kwa madarasa ya mitihani ili mikoa ya Kanda ya Ziwa Ifanye vizuri katika mitihani ya kitaifa” amesema Ndugu Kusaya.

Ndugu Kusaya amesema kuwa kuinua taalamu katika shule zote ndio kusudio la Serikali na kuwataka Wakuu wa Shule kuwasimamia vizuri walimu na wanafunzi ili waweze kufanya vizuri kitaaluma na hata kimichezo katika ngazi ya kitaifa.

Akizungumzia kuhusu upungufu wa walimu, ndugu Kusaya amesema kuwa shule nyingi zina changamoto ya uhaba wa walimu  na kuongeza kuwa tatizo la uhaba wa watumishi siyo la walimu peke yao bali ni kada zote.

Bwana Kusaya amesema kwa sasa Mkoa wa Mara una upungufu wa watumishi 15,441 wa fani mbalimbali na Serikali imekuwa ikiongeza watumishi mara kwa mara ikiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari.

Amewataka Wakuu wa Shule kuwa wabunifu kukabiliana na uhaba walimu kwa kutumia walimu wa ajira za muda mfupi wakati tatizo la uhaba wa walimu wakati linafanyiwa kazi na wamiliki wa shule hizo.

Katibu Tawala Mkoa amesema suala la uhaba wa walimu changamoto kubwa ni idadi ya watu imeoongezeka na kuibua uhaba wa watumishi na katika kukakabiliana na changamoto hiyo Serikali imekuwa ikitoa ajira mpya za watumishi kila mwaka.

Ndugu Kusaya amewataka Wakuu wa Shule kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula cha mchana shuleni kwa ushirikiano wa kamati za Shule, wazazi, viongozi na wadau  na kuzitaka Halmashauri kutumia sheria ndogondogo kufanikisha suala hilo.

Aidha, amewahimiza wazazi na walezi kuwatunza watoto wao vizuri ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanapata chakula cha mchana wakiwa shuleni ili kuboresha ufaulu na utoro shuleni.

Ndugu Kusaya amewataka Wakuu wa Shule za Serikali kusimamia miradi katika maeneo yao kwa umakini na kuwapongeza kwa kusimamia vizuri miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TAHOSA Kanda ya Ziwa alisema kuwa anaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa maboresho ya sekta ya elimu kwa kutoa posho ya madaraka na elimu bila malipo kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha sita.

“Kumekuwa na ongezeko la walimu wanaoajiriwa, kulipwa madai mbalimbali, maboresho katika mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu na maboresho ya mitaala” amesema Mwenyekiti wa TAHOSA.

Mwenyekiti huyu wa TAHOSA Kanda ameahidi kuwa wataongeza nguvu ya kuhamasisha wazazi/walezi kuhusu upatikanaji wa chakula cha mchana shuleni ili kuongeza ufaulu na kupunguza utoro.

Aidha, ameahidi kuongeza ushirikiano baina ya TAHOSSA Kanda ya Ziwa na serikali na kuongeza mafanikio zaidi ya kielimu na michezo.

Wakuu wa Shule wa Mikoa ya Geita, Mwanza na Mara walishiriki kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mwembeni Complex na kuhudhuriwa na wasimamizi wa sekta ya elimu Mkoa wa Mara na Wakuu wa Shule zaidi ya 700.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa