• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi wahimizwa kushiriki Sensa

Posted on: August 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee amewahimiza wananchi wote wa Mkoa wa Mara kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ili waweze kuhesabiwa.

Akizungumza kabla ya kuhesabiwa nyumbani kwake katika Ikulu ndogo ya Musoma leo, Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa makarani wa sensa na kutoa taarifa sahihi ili zoezi hili katika Mkoa wa Mara liweze kwenda vizuri kama inavyotarajiwa.

“Zoezi ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu kwa hiyo ninawaomba tusiiangushe Serikali, tushiriki kikamilifu na kujibu maswali yote ya Sensa tutakayoulizwa na makarani wa sensa” alisema Mheshimiwa Mzee.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa taarifa zote zitakazotolewa na wananchi kwa karani wa Sensa zitakuwa ni siri na zitatumika kwa madhumuni ya Sensa na makarani wote wamesaini kiapo cha kutunza siri za taarifa zote atakazozikusanya katika zoezi la Sensa.

Kwa upande wake, Mratibu wa Sensa katika Mkoa wa Mara Bwana Daniel Danda ameeleza kuwa zoezi limeshaanza vizuri katika Mkoa mzima wa Mara na tayari makarani wote wapo kwenye sehemu zao wanaendelea na kazi.

“Zoezi la Sensa limeanza rasmi usiku wa kuamkia leo, na tayari watu walio katika makundi maalum taarifa zao zimeshachukuliwa na kwa sasa makarani wanaendelea na zoezi la Sensa katika Kaya mbalimbali.

Bwana Danda ameeleza kuwa mpaka muda huo kulikuwa hamna sehemu ambapo zoezi la Sensa katika Mkoa wa Mara lilikuwa limekwama na kuwaomba wananchi kutoa ushirkiano kwa makarani wa Sensa ili kufanikisha zoezi hilo.

Zoezi la Sensa limeanza rasmi leo tarehe 23 Agosti, 2022 na litaendelea kwa muda usiopungua siku 10 kuanzia leo lakini taarifa zitakazotolewa ni za watu waliolala katika kaya usiku wa kuamkia tarehe 23 Agosti, 2022.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa