• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wanafunzi wapatiwe chakula shuleni- Mtambi

Posted on: May 6th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe.Kanali Evans Alfred Mtambi amesisitiza utoaji wa chakula cha mchana shuleni kwa kila mwanafunzi, huku wananchi wakiambiwa wahakikishe hilo linafanyika, shabaha ni kuongeza ufaulu na kuondoa utoro wa wanafunzi shuleni.

Haya yamesemwa Aprili 30, 2025 katika viwanja vya Mkendo Manispaa ya Musoma ambapo Kanali Mtambi alikuwa akikabidhi madawati kadhaa kwa shule za msingi na sekondari.

“Nawakumbukusha suala la chakula cha mchana mashuleni, angalau mlo mmoja, hili suala halikwepeki, hili ni lazima kwa wana Mara wote, nawaombeni tuhakikishe chakula cha mchana kinachangiwa na kila mzazi/ mlezi mwenye mtoto shuleni kwetu.

Ninaomba nisisikie ubadhilifu wa chakula hicho, ninasema wazi sitomvumilia mtu yoyote atakayefanya ubadhilifu wa chakula cha wanafunzi shuleni.”

Kanali Mtambi alisisitiza Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuhakikisha zinakamilisha kutengeneza madawati yaliyopungua na wanafunzi wa Mkoa wa Mara ni mwiko kukaa chini.

“Tangu jana nilikuwa na vikao na viongozi wezangu juu suala hili hili, nasisitiza kuwa hakuna mtu atakayevumiliwa kwa uzembe huu na ndiyo maana leo nimekuja kukabidhi madawati haya yaliyotengenezwa na wadau mbalimbali” amesema Mhe. Mtambi

Awali akisoma taarifa ya Manispaa ya Musoma Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Mwalimu Bakari Sagini alisema kuwa Manispaa ina shule 65 ambapo shule za msingi ni shule za sekondari ni 21.

Bwana Sagini ameeleza kuwa shule hizo zina wanafunzi 55,764 ambapo wanafunzi wa shule za msingi ni 38,212 na wanafunzi wa shule za sekondari ni 17,552 na Manispaa ya Musoma ina upungufu wa madawati 4,406.

 “Tunamshukuru Mbunge wa Musoma Mjini Mhe. Vedasto Mathayo na wadau wengine kwa kufanikisha zoezi hili ambalo litapunguza changamoto ya madawati katika Manispaa ya Musoma” amesema Bwana Sagini.

Hafla ya kukabidhi madawati imehudhuliwa na viongozi kadhaa wa Chama na Serikali, huku wanafunzi wa shule zinazopokea madawati hayo walikuwepo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa