• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wahusika wa vurugu Remung'oriori/Mikomalilo wakamatwe-RC

Posted on: May 15th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 14 Mei, 2024 amefanya ziara katika Vijiji vya Mikomalilo Wilayani Bunda na Remung’orori Wilaya ya Serengeti kukagua athari za vurugu zilizotokea tarehe 12 Mei, 2024 na kuliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wote waliohusika na vurugu hizo.

Mhe. Mtambi amefikia hatua hiyo baada ya kuvitembelea vijiji hivyo na kukagua athari za vurugu hizo ambapo watu tisa wamejeruhiwa na baadhi ya makazi ya muda ya wafugaji kuharibiwa katika vijiji hivyo kufuatia mgogoro wa ardhi ambao umekuwa ukiibuka na kufifia katika eneo hilo kuanzia mwaka 1954 hadi sasa. 

“Ninaagiza watu wote waliohusika katika kufanya vurugu zilizotokea tarehe 12 Mei, 2024 wakamatwe mara moja na wafikishwe mahakamani” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewataka wananchi wa vijiji hivyo kuacha kukuza mambo kuhusiana na athari za vurugu zilizotokea tarehe 12 Mei, 2024 katika eneo hilo na kuwataka kuacha kujichukulia sheria mkononi jambo ambalo amesema linasababisha vurugu ndogo kuwa jambo kubwa bila sababu.

“Hamwezi kutatua tatizo kwa kutengeneza tatizo jingine kubwa zaidi kuliko tatizo la awali, Serikali haitamvumilia mtu yoyote anayejichukulia sheria mkononi na kusababisha vurugu katika eneo hili” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amewataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kawaida katika eneo hilo wakati Serikali inaangalia ufumbuzi wa kudumu kuhusiana na mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu katika vijiji hivyo.

Akiwa katika mkutano huo, Mhe. Mtambi amewaonya wananchi wanaopenda kuanzisha vurugu katika eneo hilo kuwa watachukuliwa hatua za kisheria na mashambuliano yote katika eneo hilo ametaka yakome kuanzia sasa na Wakuu wa Wilaya za Serengeti na Bunda wasimamie amani na utulivu katika eneo hilo.

Kanali Mtambi amesema hamna sababu ya kuendelea kuukuza mgogoro huo na hamna sababu ya wananchi wa vijiji hivyo kubaguana wenyewe kwa wenyewe na kuwataka wazee wa eneo hilo kulinda amani na utulivu wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhisho la kudumu la mgogoro huo. 

Amewataka wananchi wa vijiji hivyo kupitia viongozi wa vijiji kuwasilisha maoni yao kuhusiana na mgogoro huo kwa viongozi wa Wilaya ili maoni yao yawasilishwe mkoani ili yaweze kuangaliwa na wataalamu na watapata mrejesho.

Wakati huo huo, Kanali Mtambi ametaja sababu zinazochochea migogoro ya ardhi katika Mkoa wa Mara linatokana na sehemu kubwa ya Mkoa wa Mara kuwa ni Ziwa Victoria asilimia 36 na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti asilimia 36 huku ardhi ya shughuli za kilimo, makazi, migodi, maofisi na viwanda ni asilimia 28 tu ya eneo la Mkoa wa Mara huku kukiwa na idadi kubwa ya watu.  

Mhe. Mtambi ameitaja sababu nyingine ya migogoro ya ardhi ni kuwa wafugaji wa Mkoa wa Mara hawahami kutatufa malisho mikoa mingine na hivyo kuendelea kuongeza wafugaji na mifugo wakati eneo lililopo tayari ni dogo na hivyo kuchochea migogoro ya mara kwa mara.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mikomalilo, Wilaya ya Bunda Bwana Joseph Wambura Machali ameeleza kuwa mgogoro katika eneo hilo ulikuwa umetualia hadi tarehe 12 Mei, 2024 ambapo vurugu ziliibuka katika eneo hilo.

Bwana Machali amesema chanzo cha vurugu hizo ni Bwana Magoto Magwaigu mkazi wa Kijiji cha Mikomalilo kwenda katika eneo hilo kufuata miti aliyokuwa ameikata tarehe 11 Mei, 2024 ndipo alipovamiwa na watu na akapiga yowe na watu wengine wakaja kumsaidia.

Bwana Machali ameeleza kuwa walipoona vurugu zinazidi kuongezeka wakapiga simu polisi ambao walifika wakati vurugu zikiwa zinaendelea na kusaidia kuzima vurugu hizo.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mtambi ameambatana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya za Bunda na Serengeti, baadhi ya maafisa kutoka Sektretarieti ya Mkoa, Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara na maafisa kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa