• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wadau, Wananchi, Viongozi Tuuhifadhi Mto Mara

Posted on: September 14th, 2021

Uongozi wa Mkoa wa Mara umewataka wadau, wataalamu na wananchi kuongeza juhudi katika kuhifadhi ikolojia ya Bonde la Mto Mara kwa maendeleo ya kiutalii ya nchi za Tanzania na Kenya.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Lt. Col. Michael Mangwela Mtenjela wakati akizindua rasmi maadhimisho ya 10 ya Mto Mara mwaka 2021 katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Tarime leo tarehe 14 Septemba 2021.

“Tunatakiwa kuongeza nguvu katika kuhifadhi ikilojia ili tuweze kuulinda Mto Mara kwa sababu hifadhi zetu za Serengeti na Masai Mara zinategemea sana uwepo wa Mto Mara na hifadhi hizi ni tegemeo la kiuchumi kwa nchi zetu za Kenya na Tanzania” amesema Mheshimiwa Mtenjela.

Mheshimiwa Mtenjela amesema wananchi wanaopitiwa na Mto Mara ni wanafuika wakubwa wa mto huu lakini hawana elimu ya uhifadhi wa mazingira hivyo ni muhimu wadau na wataalamu wakatoa  elimu ya uhifadhi ili wananchi waweze kusaidia katika kutunza mto huu.

Mheshimiwa Mtenjela ameeleza kuwa katika kuadhimisha Siku ya Mto Mara mwaka 2021, Mkoa wa Mara umepanda miti 13,000 na kuweka vigingi 70 katika vijiji vya Mrito na Kerende vilivyopo katika Wilaya ya Tarime.

Mheshimiwa Mtenjela ameeleza kuwa idadi ya miti na vigingi imeongezeka ikilinganishwa na mwaka 2020 ambapo miti 2600 ilipandwa pamoja na vigingi 20 katika Wilaya ya Butiama.

“Ongezeko la upandaji miti linatokana na juhudi za maksudi zinazochukuliwa na Mkoa wa Mara katika kuhifadhi ikolojia ya Bonde la Mto Mara na Mkoa mzima wa Mara” alisema Mheshimiwa Mtenjela.

Mheshimiwa Mtenjela ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime ameeleza kuwa japokuwa katika tukio la kuhama kwa nyumbu kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwenda Hifadhi ya Masai Mara Wilaya ya Tarime haitajwi, lakini Wanyama wakitoka Serengeti ni lazima wapite katika Wilaya ya Tarime kabla ya kuvuka mpaka.

Mto Mara unaanzia katika milima ya Mau nchini Kenya na unamwaga maji yake katika Ziwa Victoria.

Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mara kinatarajiwa kuwa tarehe 15 Septemba 2021 na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo atakuwa Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso (Mb.).

Kauli mbiu ya maadhimisho ya 10 ya Siku ya Mara mwaka 2021 ni Tuhifadhi Mto Mara kwa Utalii na Uchumi Endelevu.    

Uzinduzi wa maadhimisho hayo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Wizara ya Maji, Wizara ya Maliasili na Utalii, taasisi mbalimbali za serikali, viongozi wa Mkoa na Wilaya, Asasi zisizo za kiserikali, sekta binafsi na wananchi.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa