• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Viongozi wakagua Kituo cha Pilisi Wilaya ya Butiama

Posted on: November 19th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda  leo tarehe 19 Novemba, 2023 amepokea taarifa na kukagua ujenzi wa Kituo Cha Polisi Wilaya ya Butiama kinachoendelea kujengwa katika Wilaya ya Butiama.  

Akizungumza  na Waandishi wa Habari mara baada ya kukagua na kupokea maelezo ya mradi huo, Mhe. Mtanda amesema “ujenzi huo mpaka sasa umegharimu shilingi milioni 366 na umejenga jengo lenye vyumba 25 vya ofisi, mahabusu sita na vyoo 13”.  

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa ziara yake ya kukagua ujenzi huo imetokana na taarifa iliyotolewa katika mitandao ya kijamii kuwa ujenzi huo umegharimu shilingi milioni 802 taarifa ambayo amesema sio sahihi kwa hatua za ujenzi wa jengo hilo zilipofikiwa kwa sasa.  

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa mradi wa ujenzi wa jengo la Kituo cha Polisi Wilaya ya Butiama, ni wa daraja Daraja B, una jengo moja lenye mita za mraba 737.2 na mpaka utakapokamilika ndio umekadiriwa kutumia shililingi milioni 802.

Aidha, Mhe. Mtanda ameagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kutuma wataalamu wake kufanya uchunguzi wa mradi huo Jumatatu tarehe 20 Novemba, 2023 ili kuweza kubaini uhalali wa fedha zilizotumika na fedha za kukamilisha mradi huo zilizoombwa kutoka Makao Makuu ya Jeshi ya Polisi.   

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa,  Afisa Miliki wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara Bwana Charles Mwenya ameeleza kuwa gharama za mradi huo hadi utakapokamilika itakuwa ni shilingi milioni 802 lakini mpaka sasa fedha iliyopokelewa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara ni shilingi milioni 500.

Bwana Mwenya ameeleza kuwa kazi zilizofanyika mpaka sasa ni kuchimba kisima cha kutunza maji, kujenga jengo na kuezeka, kuweka flemu za milango, kupiga ripu, kujenga mabenchi ya mahabusu, kufanya wiring, kuweka magriri ya madirisha na dari maalum kwenye vyumba vya mahabusu.  

Bwana Mwenya ameeleza kuwa mradi huo wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Butiama umeanza rasmi tarehe 6 Mei, 2023 na unategemewa kukamilika Desemba, 2023 na unatekelezwa kwa njia ya nguvu kazi yaani force account.

Ziara hiyo ilihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Butiama (CCM) na Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mwl. Moses Kaegele, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara ASP. Salim Morcase na Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Butiama.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa