• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Viongozi na Watumishi Mara watoa zawadi kwa wahitaji

Posted on: December 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo tarehe 24 Desemba, 2022 amekabidhi zawadi kwa wahitaji wanaoishi katika vituo vitatu vya kulelea watu wanaoishi katika mazingira magumu zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni tatu zilizotokana na michango ya viongozi na watumishi wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mheshimiwa Mzee ameeeleza wazo la kutoa zawadi hizo lilitokana na kitendo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa zawadi kwa ajili ya wahanga wa ukatili katika Kituo cha Masanga.

“Moyo wa Mheshimiwa Rais kutoa msaada kwa vituo mbalimbali wakati huu umetuhamasisha na sisi kutoa msaada kwa wenye uhitaji wanaoishi katika vituo vingine vilivyopo katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewashukuru sana viongozi na watumishi wote walioitikia wito wa kuchangia fedha za kununua zawadi hizo na kuahidi wakati mwingine michango itaanza mapema zaidi na kuwashirikisha watu wengi zaidi.

Mheshimiwa Mzee amewataka wananchi kutoa msaada wa hali na mali kwa vituo vinavyohifadhi watu wanaoishi katika mazingira magumu ili viweze kuwahudumia wahitaji wengi zaidi.  

Vituo vilivyopewa zawadi ya sikukuu ni pamoja na Musoma Children Home kilichopo katika Wilaya ya Musoma, Kituo cha Kulelea Wazee cha Nyabange na Kituo cha Nyumba Salama cha Matumaini ambacho kinawahifadhi watoto ambao ni wahanga wa ukatili vilivyopo katika Wilaya ya Butiama.

Zawadi za sikukuu zilizotolewa katika vituo hivyo ni pamoja na mbuzi, mchele, maharage, mahindi, pampasi, viungo, taulo za kike na sabuni.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu, Katibu Tawala wa Wilaya ya Butiama, Kaimu Mkurugezi wa Wilaya ya Butiama na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wilaya ya Musoma na Wilaya ya Butiama. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa