• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Uthamini wa eneo la Nyatwali umefikia zaidi ya asilimia 50

Posted on: January 26th, 2023

Zoezi la uthamini katika eneo la Ghuba ya Speke, katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi endelevu wa mfumo wa ikolojia wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na usalama wa wananchi linaendelea vizuri na kwa sasa limefikia asilimia 53.7 ya utekelezaji wake.

Akizungumza katika Kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa zoezi la uthamini leo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu amewataka wataalamu wanaofanya uthamini huo kutoa taarifa za maendeleo ya kazi kila wiki kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kupata uelewa wa pamoja na kutoa mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa zoezi hilo Serikalini.    

“Ninataka kuanzia sasa, kila wiki Mkoa upate taarifa ya maendeleo ya zoezi la uthamini ili Mkoa uweze kupeleka taarifa za utekelezaji wa uthamini na maendeleo ya zoezi hili kila wiki” amesema Bwana Makungu.

Aidha Bwana Makungu amewataka wataalamu hao kuongeza kasi ya kufanya tathmini ili zoezi hilo liweze kukamilika kwa haraka na wananchi wa eneo la Nyatwali waweze kulipwa fidia zao na kuendelea na shughuli zao za kawaida.  

Taarifa ya wataalamu inaonyesha kuwa mpaka hadi kufikia tarehe 25 Januari, 2023 jumla ya wananchi 2,175 wametambuliwa na kufanyiwa uthamini kati ya watu 4,050 waliokadiriwa hapo awali ambayo ni sawa na asilimia 53.7 ya uthamini wote.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa zoezi la uthamini lilianza Novemba, 2022 na linatarajiwa kukamilika Machi, 2023 na mpaka sasa jumla ya fomu 2,822 kati ya 4,050 zilizokadiriwa zimechukuliwa na wananchi ambayo ni sawa na asilimia 69.68 ya makadirio ya awali.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi la uthamini katika eneo hilo ni la hiari na kabla ya kuanza lilitanguliwa na mikutano na vikao vya uhamasishaji kwa viongozi na wananchi wa Kata ya Nyatwali na Wilaya ya Bunda kwa ujumla.

Utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri wa kutwaa eneo la Ghuba ya Speke lenye ukubwa wa ekari 14,250 kwa manufaa ya umma unahusisha Mitaa ya Tamau, Nyatwali, Kariakoo na Serengeti iliyopo katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda katika Mkoa wa Mara.

Utwaaji wa eneo la Ghuba ya Speke, utaunganisha Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Ziwa Victoria na kuongeza ukubwa, uzuri wa mandhari ya vivutio vya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.  

Kikao cha kupokea maendeleo ya uthamini kimehudhriwa pia na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Wakuu wa Idara na Vitengo vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na baadhi ya wataalamu wa wanaohusika na zoezi la uthamini katika Ghuba ya Speke.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa