• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Ufisadi wabainika ulipaji wa fidia Nyamongo

Posted on: June 15th, 2020

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara imebaini kuwepo kwa ufisadi wa bilioni 3.2 katika malipo ya fidia ya ardhi katika mgodi wa Barrick North Mara katika Wilaya ya Tarime.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Alex J. Kuhanda imeeleza kuwa taasisi yake imethibitisha kuwepo kwa malipo hewa yenye thamani ya shilingi 3,271,038,570.28 na uchunguzi bado unaendelea.

“Katika uchunguzi wetu kupitia tuhuma 60 tulizozifanyia kazi tumeweza kuthibitisha kuwepo kwa ufisadi mkubwa uliochochewa na uthamini uliojaa rushwa” alisema Bwana Kuhanda.

Aidha amefafanua kuwa katika tuhuma hizo 60 TAKUKURU imebaini kuwa malipo halali kwa wananchi yalikuwa shilingi 226,858,656.52 tu na sio 3,482,988,360 zilizolipwa kama fidia kwa nyumba 72 ambazo uchunguzi umethibitisha kuwa ni hewa.

Bwana Kuhanda ameeleza kuwa kati ya malipo hayo shilingi 2,127,236,784 ilikuwa ni malipo ya fidia kwa nyumba na shilingi 1,143,796,786.28 ilikuwa ni malipo ya posho ya usumbufu na kuhama kutoka katika nyumba ambazo hazipo na hazikuwahi kuwepo.  

Bwana Kuhanda ameeleza kuwa msingi wa uchunguzi wa TAKUKURU ulilenga kujua kama ni kweli kulikuwa na malipo yaliyokuwa yanafanyika kwa tathmini ya mali hewa.

Kwa upande wake mwakilishi wa mgodi wa Barrick North Mara ameeleza kuwa hadi tarehe 9 Juni 2020 wananchi 1498 walikuwa wameshalipwa na wananchi 142 walikuwa bado wanaendelea kulipwa.

Ameeleza kuwa katika mchakato mzima iliundwa kamati ya usimamizi ambayo ilihusisha watendaji kutoka katika ngazi ya Mkoa, Wilaya na vijiji vilivyonufaika na fidia hiyo.

Aidha alieleza kuwa Mgodi huo unashukuru sana kwa ushirikiano wa kamati hiyo katika kufanikisha zoezi hilo la fidia kwa wananchi.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa TAKUKURU waliagizwa kushughulikia tuhuma za ufisadi wa shilingi bilioni 5.1 kutoka malipo hewa na malipo yaliyoongezwa.

“Uchunguzi umeonyesha kulikuwa na vyote viwili, malipo hewa kabisa na mengine yaliyoongezwa thamani ili kuwanufaisha mafisadi wachache” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha ameeleza kuwa uchunguzi huo umebaini kuna baadhi ya nyumba ni mbovu sana wenyenyumba hizo wamelipwa pesa kubwa ikilinganishwa na nyumba nyingine ambazo ni nzuri lakini wamepewa malipo kidogo.

Mheshimiwa Malima amewapongeza maafisa kutoka TAKUKURU, Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa kufanikisha zoezi hilo muhimu sana kwa mustakabali wa taifa la Tanzania.  

 Wananchi 1639 wa vitongoji vinne vya vijiji vya Matongo na Bichune walianza kulipwa fidia iliyokadiriwa ya shilingi bilioni 33 kuanzia tarehe 20 Mei 2020 na tayari wengi wao wameshalipwa ambapo ndani yake TAKUKURU imebaini udanganyifu huo na uchunguzi bado unaendelea.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa