• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Ufaulu wa Darasa la Saba wapanda Mara

Posted on: November 25th, 2023

Ufaulu wa Mtihani wa Taifa wa Kumaliza Shule ya Msingi (PSLE) katika Mkoa wa Mara kwa mwaka 2023 umepanda ambapo jumla ya watahiniwa 52,731 sawa na asilimia 75 ya watahiniwa wote 70,182 waliofanya mtihani huo wamefaulu kwa kupata madaraja A, B na C.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Makwasa Bulenga imeeleza kuwa kati ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo kwa mwaka 2023 wavulana ni 26,438 na wasichana ni 26,288.

Bwana Makwasa ameeleza kuwa mwaka 2022 Mkoa wa Mara ulikuwa na watahiniwa waliofaulu walikuwa 57,393 sawa na asilimia 74.53 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani, ukilinganisha na mwaka huu ufaulu wa mwaka huu umepanda kwa asilimia 0.47.  

“Wanafunzi wote walioanza darasa la kwanza mwaka 2017 walikuwa 90,300 ambapo kati yao wavulana walikuwa 44,900 na wasichana walikuwa 45,406 hata hivyo wanafunzi waliofanya mtihani huo walikuwa 70,182” amesema Bwana Bulenga.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa jumla ya watahiniwa 3,258 ambao ni sawa na asilimia 5.96 waliokuwa wameandikishwa kufanya mtihani katika Mkoa wa Mara hawakufanya kutokana na sababu mbalimbali.

Taarifa ya Bwana Bulenga imeitaja Halmashauri iliyofanya vizuri katika mtihani huo kuwa ni Manispaa ya Musoma, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Halmshauri nyingine ni Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Halmashauri ya Mji wa Bunda na ya mwisho ni Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.  

Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi umefanyika hapa nchini tarehe 13-14 Septemba, 2023 na matokeo yake kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) tarehe 25 Novemba, 2023.

Wakati huo huo, Baraza la Mtihani la Tanzania limefungia vituo vya mtihani viwili (02) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara vilivyothibitika kupanga kufanya udanganyifu katika mtihani huo mpaka hapo Baraza litakapojiridhisha kuwa ni salama kwa uendeshaji wa Mitihani ya Taifa.

Taarifa ya Baraza la Mitihani kuhusu matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba,2023 imeeleza kuwa  Baraza limechukua hatua hiyo kwa mujibu wa Sheria za Mitihani na kifungu 4 (8) cha Kanuni za Mitihani za Mwaka 2016.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa