• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tumuombee Mhe. Samia: Malima

Posted on: April 8th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kigoma Ali Malima amewataka watanzania kuendelee kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ili aweze kuendeleza mazuri yote aliyokuwa akiyafanya marehemu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mheshimiwa Malima amesema hayo wakati wa maombi maalum ya kumuombea Dkt. Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan yaliyoandaliwa na Kamati ya Maridhiano na Amani ya Mkoa wa Mara yaliyofanyika leo tarehe 7 Aprili 2021 katika Uwanja wa Mkendo, Manispaa ya Musoma.

“Tuendelee kumuombea Rais Samia ili awezekupata nguvu, ujasiri na uthubutu zaidi wa kuweza kuinyanyua Tanzania juu kimaendeleo” alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa wakati tunaomboleza kifo cha Magufuli tuliona tumuombee pia Mheshimiwa Samia ili Tanzania iimarike zaidi kimaendeleo chini ya uongozi wake.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa Marehemu Magufuli ameacha alama kubwa katika maendeleo ya Mkoa wa Mara na nchi ya Tanzania na mambo aliyoyafanya ni mengi ambayo yameacha historia kubwa kwa nchi yetu.

Wakati huo huo Mheshimiwa Malima amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuachana na ukabila ambao unarudisha nyuma maendeleo ya mkoa huu na badala yake wananchi waungane katika kuiletea Mara Maendeleo.

“Mheshimiwa Magufuli alipokuja hapa mara ya mwisho katika uwanja huu huu (Mkendo) alituasa kuachana kabisa na ukabila kwani hauna tija yoyote katika maendeleo ya sisi wenyewe au ya mkoa wetu” alisema Mheshimiwa Malima.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano na Amani ya Mkoa wa Mara Askofu Jacob Lutubija amewataka watu wote kumuombea Dkt. Magufuli ili Mungu aweze kumsamehe makosa yake na kumpumzisha katika amani yake. 

“Wakati tunamuombea Dkt. Magufuli, ni wajibu wetu pia kumuombea Mheshimiwa Rais ili aweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu kwa manufaa ya Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla” alisema Askofu Lutubija

Kamati ya Maridhiano na Amani inaundwa na viongozi mbalimbali wa madhehebu ya dini za kiislamu na kiktristu yaliyopo katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa