• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tumieni Mara Day 2020 kujifunza Kilimo

Posted on: September 11th, 2020

Wananchi wa Mkoa wa Mara wametakiwa kutumia maadhimisho ya Mara Day 2020 ili kujifunza mbinu bora za kilimo zitakazowasaidia kuwakomboa kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake kuhusiana na maadhimisho ya Mara Day 2020 ambayo kwa upande wa Tanzania yatafanyika katika viwanja vya Mama Maria Nyerere vilivyopo katika Kitongoji cha Nyamigembe, Kijiji cha Butiama, wilayani Butiama kuanzia tarehe 12 hadi 15 Septemba 2020.

“Mwaka huu tumeunganisha Mara Day na maonesho ya kilimo, wananchi tutumie fursa hii kujifunza kuhusu kilimo bora na endelevu chenye tija ili tuweze kujikwamua kiuchumi” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha amewataka wakulima kutembelea na kupata mafunzo katika uwanja huo kwa mwaka mzima ili kuweza kupata mafunzo na ushauri kuhusu kilimo, ufugaji na uvuvi ili kuweza kuongeza tija katika shughuli zao.

Mheshimiwa Malima asemma shughuli zitakazofanyika katika Mara Day 2020 ni pamoja na upandaji miti na uwekaji wa becon katika eneo la Kirumi, kongamano la kimtandao litakalohusisha wadau kutoka Kenya na Tanzania, maonyesho na mafunzo ya kilimo yatakayofanyika katika viwanja vya maonyesho ya kilimo Butiama.

Mheshimiwa Malima pia amewataka wananchi wanaouzunguka Mto Mara kupunguza shughuli za kibinadamu katika eneo la mita sitini kuzunguka bonde la mto huo kwa mujibu wa sheria ya rasilimali za maji.

“Nimesikitishwa sana na ile clip inayoonyesha mwekezaji akiwafukuza wanyama wanaovuka Mto Mara kwenda Masai Mara nchini Kenya, lakini kama wadau tulikubaliana kuhusu kutoruhusu shughuli za kibinadamu kwenye kingo la Mto Mara ninategemea Serikali ya Kenya itachukua hatua za haraka kudhibiti hali hii” alisema Malima.

Uwanja wa maonyesho wa Mama Maria Nyerere una eneo la 120 umeandaliwa na Serikali ya Mkoa wa Mara kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wakulima ambalo limegawanyika katika maeneo ya ufugaji, uvuvi, kilimo na sehemu ya mafunzo.  

 Mara Day ni maadhimisho ya kuhamasisha shughuli za uhifadhi katika Bonde la Mto Mara ambalo linafanyika kwa kupokezana katika nchi za Kenya na Tanzania tangu mwaka 2012 na kilele ni tarehe 15 Septemba ya kila mwaka.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa