• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TASAF Yatoa bilioni 48.7 Kunusuru Kaya Maskini Mara

Posted on: August 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee ameeleza kuwa hadi kufikia tarehe 15 Agosti, 2022 jumla ya bilioni 48.7 zimekwishatolewa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kupitia Mpango wa Kususuru Kaya Maskini katika Mkoa wa Mara kuanzia mwaka 2014 hadi sasa.

Akitoa taarifa kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Kufuatilia Ofisi za Viongozi wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi na Maafisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili ya Rais, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa una wanufaika kaya 63,346 kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kati ya fedha zilizotolewa, bilioni 42.856 ni kwa ajili ya malipo ya walengwa, shilingi bilioni 5.844 ni kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji ngazi ya Mkoa, Halmashauri, Kata na ngazi ya Mitaa/Vijiji na shilingi milioni 283.542 ni kwa ajili ya miradi miwili ya maendeleo.

Katika taarifa hiyo, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa uzinduzi wa utekelezaji wa sehemu ya pili ya TASAF awamu ya III ulifanyika tarehe 10 Agosti, 2021 katika Mkoa kwa lengo la kufikia asilimia 30 ya vijiji na mitaa ambayo haikuwa imefikiwa na sehemu ya kwanza ya TASAF III.

Mheshimiwa Mzee ameeleza kuwa kwa sasa jumla ya vijiji na mitaa 792 kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara zimeingia katika mpango huo huku vijiji 13 katika Wilaya ya Bunda (03) na Serengeti (10) havijafikiwa na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Kusimamia Ofisi za Viongozi ya Baraza la Wawakilishi, Zanzibar Mheshimiwa Machano Othman Said amewataka wanufaika wa Mpang wa Kunusuru Kaya Maskini kutumia fedha wanazopata vizuri kwa maendeleo yao.

“Hii fedha mnayoipata mkiitumia vizuri itawasaidia sana katika kujiletea maendeleo yenu binafsi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla” ameeleza Mheshimiwa Said.

Mheshimiwa Said ameeleza kuwa viongozi wa Serikali wanapambana kuhakikisha fedha hizo zinapatikana na kwamba wanufaika wakizitumia vizuri wataweza kufanya maendeleo yao na kuwatoa kabisa katika hali ya umaskini waliyokuwa nayo hapo awali.

Katika ziara hiyo, Viongozi hao walitembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama, wanufaika wa Kijiji cha Mlyaze katika Wilaya ya Butiama, Makumbusho ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Nyumbani kwa Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Butiama.  

 Katika ziara hiyo, viongozi hao waliambatana na maafisa wa TASAF kutoka Makao Makuu Dodoma, maafisa wa TASAF Mkoa wa Mara, maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Wilaya ya Butiama na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa