• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tarime Mji malizaneni na wananchi- Hapi

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Mji wa Tarime kurudisha fedha za wananchi au kuwapa maeneo ya kujenga vibanda vya biashara walivyoahidiwa ndani ya mwezi mmoja.

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 13 Agosti 2021 na Mheshimiwa Hapi wakati akizungumza na viongozi na watumishi wa Wilaya ya Tarime katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Tarime.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Tarime kusimamia suala hilo na kuhakikisha wananchi wa Tarime wanapata haki yao ndani ya mwezi mmoja.

Awali akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye maarufu kama namba tatu ameeleza kuwa Halmashauri hiyo iliwachangisha watu fedha shilingi 450,000 mwaka 2017 kwa ahadi ya kupewa vibanda vya biashara.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tangu wakata huo mpaka leo wananchi hawajapata vibanda wala hamna majibu ya kueleweka kuhusu fedha zao walizotoa” alisema Mheshimiwa Kiboye.

Mheshimiwa Kiboye ameeleza kuwa matatizo kama hayo yanawachonganisha wananchi na Chama cha Mapinduzi kwa sababu ya uzembe wa watendaji wachache wanaichafua serikali.

Akizungumzia suala hilo Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Tarime Bwana Erasto Mbunga ameeleza kuwa wakati viwanja hivyo vya biashara vinatangazwa takriban wananchi 80 walilipia ambao bado wanadai mpaka sasa.

Bwana Mbunga ameeleza kuwa kwa sasa mradi huo ambao awali walipanga kuutekeleza ulisitishwa na serikali na kupangiwa majukumu mengine na hivyo bado walikuwa wanaangalia utaratibu wa kuwalipa wananchi.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mheshimiwa Mwita Waitara ambaye pia ni Mbunge wa Tarime Vijijini kupitia Chama cha Mapinduzi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa