• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tamisemi yazitaka Shule za Ufundi Kufundisha kwa Vitendo

Posted on: January 22nd, 2021

Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mheshimiwa Suleiman Jafo amezitaka shule za sekondari za ufundi zilizopo hapa nchini kutoa elimu kwa vitendo, kufanyakazi kwa weledi na ubinifu ili kuweza kuwaandaa wanafunzi wanaosoma katika shule hizo kwa ajili ya Tanzania ya Viwanda.

Mheshimiwa Jafo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Maafisa Elimu wa Mikoa, Halmashauri na Wakuu wa Shule na walimu wapya walioajiriwa katika shule tisa za sekondari za ufundi zilizopo hapa nchini leo tarehe 22 Januari 2021 kupitia mtandao wa video.

“Shule hizi kwa sasa zimeboreshwa sana kuanzia miundombinu hadi wataalamu wa kufundisha hivyo ni matarajio yetu (TAMISEMI) kuwa zitajikita zaidi kwenye kufundisha kwa vitendo ili vijana wanaofundishwa watoke wakiwa wanaujuzi wa kutosha kuweza kutumika kwenye Tanzania yaViwanda” alisema Mheshimiwa Jafo.

Mheshimiwa Jafo ameeleza kuwa wakati serikali ya awamu ya tano inaingia madarakani kwa mara ya kwanza, shule hizi zilikuwa na miundombinu chakavu, hazina walimu wenye utaalamu wa ufundi na hazikuwa na vifaa vya kufundishia.

Mheshimiwa Waziri ameeleza kuwa kwa sasa shule hizi zimekarabatiwa na serikali imetumia shilingi zaidi ya shilingi bilioni 16 kukarabati shule hizi tayari serikali imeajiri wataalamu 150 wa ufundi mbalimbali kuanzia Novemba 2020 ambao tayari wapo mashuleni ili kuboresha ufundishaji katika shule hizi za ufundi.

Aidha Mheshimiwa Jafo ameahidi serikali kupeleka shilingi milioni 30 kwa kila shule ya ufundi kwa ajili ya kununua au kukarabati vifaa vya kujifunzia na kufundishia ili kuimarisha elimu inayotolewa katika shule hizo.

Aidha amezitaka halmashauri kuwalipa mara moja posho ya kijikimu walimu wote waliopangiwa katika hizi shule za ufundi ili waweze kujikimu wakati jitihada za kuingizwa katika mifumo ya mishahara zikiwa zinaendelea.

Mheshimiwa Waziri pia amewataka Wakuu wa Mikoa ambapo shule hizo zipo wawe walezi wa shule hizo na kusisimamia kwa ukaribu shule hizi ili ziweze kuleta manufaa yanayotarajiwa katika mikoa yao.

Mheshimiwa Jafo pia amewataka Wakuu wa Shule za Ufundi kuwahusisha mafundi mahiri waliopo katika mikoa yao katika ufundishaji wa wanafunzi kwa vitendo  ili wanafunzi wanaosoma katika shule hizi waweze kufaidika na umahiri wa mafundi hao.   

 Shule za sekondari za ufundi hapa nchini ni pamoja na Shule ya Ufundi Chato (Geita), Shule ya Ufundi Mwadui (Shinyanga), Shule ya Ufundi Musoma (Mara), Shule ya Ufundi Moshi (Kilimanjaro) na shule ya Ufundi Bwiru (Mwanza). Shule nyingine ni Shule ya Ufundi ya Tanga (Tanga), Shule ya ufundi Iyunga (Mbeya), shule ya Ufundi Ifunda (Iringa) na  Shule ya Ufundi Mtwara (Mtwara).  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa