• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAMISEMI Yasistiza matumizi ya GoTHOMIS

Posted on: November 25th, 2022

Mkurugenzi wa Huduma za Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI), Dkt. Ntuli Kapologwe leo amefanya kikao cha majumuisho na wasimamizi wa sekta ya afya na wadau wa afya wa Mkoa wa Mara na kuwataka Waganga Wakuu wa Halmashauri kufunga mfumo wa ukusanyaji wa mapato katika vituo vya kutolea huduma za afya (GoTHOMIS).

Akizungumza katika kikao hicho baada ya ziara aliyoifanya katika Mkoa wa Mara, Dkt. Kapologwe ameipongeza Manispaa ya Musoma kwa kuboresha makusanyo katika vituo vya kutolea huduma za afya kutoka shilingi 37,210,000 mwaka 2017/2018 hadi 396,410,000 mwaka 2021/2022.

“Haya mafanikio yamekuja baada ya Manispaa ya Musoma kufunga mfumo wa kukusanyia mapato katika vituo vya kutolea huduma za afya (GOTHOMIS) katika vituo vyake na kuboresha makusanyo” alisema Dkt. Kapologwe.

Aidha, amekipongeza Kituo cha Afya cha Natta katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa kuongeza mara dufu ukusanyaji wa mapato baada ya kufunga GoTHOMIS akilinganisha na hospitali ya Wilaya ya Serengeti ambayo haijafunga mfumo huo na kukusanya mapato kidogo huku ikiwa na watu wengi zaidi wanaopatiwa huduma.

Aidha, ameupongeza Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri unayoendelea kuifanya katika sekta ya afya hususan katika utoaji wa chanjo ya UVIKO 19 ambapo kwa sasa Mkoa wa Mara umeshika nafasi ya 9 kitaifa katika utoaji wa chanjo hiyo.

Dkt. Kapologwe amewataka Waganga Wakuu wa Halmashauri kushughulikia mapungufu yote yaliyoonekana wakati wa ziara hiyo na kuhakikisha kuwa mapungufu kama hayo yanatatuliwa katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya wa Mkoa wa Mara Dkt. Juma Mfanga ameishukuru timu ya wataalamu kutoka TAMISEMI kwa ziara na maelekezo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo hayo.

“Tunaahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na tutawasilisha taarifa ya utekelezaji wa maelekezo hayo” alisema Dkt. Mfanga.

Wakati huo huo, Dkt. Mfanga ambaye ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara ameishukuru AMREF kwa kuleta wataalamu wa afya 385 wa kada mbalimbali ili kusaidia kuboresha huduma za afya katika Mkoa wa Mara.

Aidha, Dkt. Mfanga amewashukuru wasimamizi wa sekta ya afya kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kwa kuitikia wito wa kikao hicho na kufika kwa wingi na kuwataka kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa kwa haraka.

Katika ziara hiyo, timu ya wataalamu imefanya ziara ya siku tatu na kutembelea vituo vya kutolea huduma za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Halmashauri ya Mji wa Bunda, Manispaa ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa