• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAMISEMI yaitaka Mara kuboresha ufaulu

Posted on: April 28th, 2020

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mara kuboresha kiwango cha ufaulu katika mitihani ya taifa kwa shule za msingi na sekondari. 

Eng. Nyamhanga ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti tofauti katika ziara yake ya siku tatu ya kutembelea Mkoa wa Mara na kukagua maendeleo katika sekta ya Elimu, Afya na utayari wa Mkoa katika kukabiliana na janga la homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

“Tumeiona mipango yenu na utekelezaji wake umeanza lakini tunahitaji ufaulu upande. Na sisi kwa upande wa wizara tumembadilisha Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara labda tutakuja kupata matokeo mazuri wakati huu” alisema Eng. Nyamhanga.

Katika kuunga mkono juhudi mbalimbali za wananchi na watendaji wa Mkoa wa Mara, Katibu Mkuu TAMISEMI aliahidi kutoa fedha za kusaidia ukamilishaji wa maboma ya madarasa, nyumba za walimu na maabara katika shule mbalimbali alizozitembelea katika ziara hiyo.

Katika ziara yake ya Mkoa wa Mara, Katibu Mkuu TAMISEMI alitembelea shule za sekondari za Kebogwe, Tarime na Nyamigwela na Shule ya Msingi ya Nyasaricho katika wilaya ya Tarime; Sekondari za Mapinduzi, Mugumu na Natta katika Wilaya ya Serengeti; na Sekondari ya Kabasa katika Wilaya ya Bunda.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula ameahidi Mkoa kufanya vizuri kutokana na jitihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na serikali pamoja na wadau wa Elimu katika Mkoa wa Mara.

“Kwa niaba ya watendaji wote wa Mkoa huu, tunashukuru sana wadau wetu mbalimbali ambao wamekuwa wakiunga mkono uboreshaji wa elimu katika Mkoa wa Mara” alisema Bibi Mthapula.

 Katibu Mkuu TAMISEMI ametembelea wilaya za Tarime, Serengeti na Bunda katika Mkoa wa Mara kukagua shughuli za maendeleo katika sekta za Afya, Elimu na kuangalia utayari wa mkoa katika kukabiliana na janga la Korona.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa