• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU yatoa taarifa ya utekelezaji

Posted on: July 29th, 2022

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara leo tarehe 28 Julai, 2022 imetoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yake katika robo ya Aprili hadi Juni, 2022 na kueleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU imefuatilia utekelezaji wa miradi 24 ya maendeleo.  

Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Antony Gang’olo, ameeleza kuwa miradi iliyofuatiliwa ilikuwa na thamani ya shilingi 18,578,309,485 katika sekta za afya, barabara, maji na elimu.

“Katika ukaguzi huo, miradi mitatu ilibainika kuwa na changamoto ambazo zinaendelea kurekebishwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa chumba cha wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime; mradi wa maji wa Kijiji cha Robanda na mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Sekondari ya Mapinduzi katika Wilaya ya Serengeti” alisema Gang’olo.

Aidha, Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU imetembelea klabu za wapinga rushwa 86 katika Wilaya zote sita na kufanya mikutano ya hadhara 30 katika vijiji, mitaa na vitongoji mbalimbali katika Mkoa wa Mara.  

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho pia TAKUKURU imeshiriki katika vikao 15 na kutoa mada za kuelimisha umma pamoja na kushiriki vipindi vitatu katika vituo vya redio za kijamii za Victoria FM, Mazingira FM na Bunda FM.

Wakati huo huo, Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho, jumla ya malalamiko 106 na kati ya malalamiko hayo 79 yalihusu vitendo vya rushwa yanaendelea kufanyiwa kazi wakati 27 hayakuhusu vitendo vya rushwa.

“Kati ya malalamiko hayo, malalamiko 26 yalihusu TAMISEMI, 11 Afya, 07 Jeshi la Polisi, 06 sekta ya vuvi, 06 sekta ya ardhi na sekta nyinginezo” alisema Bwana Gang’olo.  

Bwana Gang’olo ameeleza kuwa katika kipindi hicho, uchunguzi katika majalada 18 ulikamilika na kesi 18 zilifunguliwa mahakamani na kufanya kesi zinazoendelea mahakamani kuwa 36 huku kesi tatu zikiamriwa ambapo kesi 2 washtakiwa walipatikana na hatia na kesi moja mshtakiwa aliachiwa huru.  

Ameeleza kuwa katika kipindi cha Julai- Septemba 2022 TAKUKURU Mkoa wa Mara itaongeza nguvu zaidi katika kuzuia vitendo vya rushwa na itashirikiana na Chama cha Skauti Tanzania kutekeleza mpango wa TAKUSKA unaolenga kutoa elimu ya rushwa kwa vijana wengi zaidi.  

Taarifa hii ya TAKUKURU ni mwendelezo wa taarifa zinazotolewa na TAKUKURU Mkoa wa Mara kwa waandishi wa habari kila baada ya miezi mitatu.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa