• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU yafuatilia miradi ya maendeleo 32 Mara

Posted on: April 25th, 2024

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara leo imetoa taarifa yake ya  utendaji kwa kipindi cha Januari, 2024 hadi Machi, 2024 ambapo imefuatilia miradi ya maendeleo 32 yenye thamani ya shilingi 11,372,416,636.5 inayotekelezwa na Serikali katika sekta za elimu, afya, barabara na maji.

Taarifa iliyotolewa leo na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Mohamed Shariff imeeleza kuwa uchunguzi wa awali ulibaini dosari katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Bunda yenye thamani ya shilingi bilioni nne.

“Tayari Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imerekebisha dosari zilizoonekana ikiwa ni pamoja na kuta zilizokuwa zimepinda kwenye vyumba vya madarasa, nyufa kwenye mabweni, fundi amekatwa shilingi 360,000 kufidia simenti iliyotumika kutengeneza ukuta mnene uliozidi katika ujenzi wa bweni na vitabu vya stoo vilivyokuwa havijazwi kwa sasa vinajazwa” amesema Bwana Shariff.

 TAKUKURU imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kuyafanyia kazi mapungufu yaliyoonekana kwa wakati hata hivyo uchunguzi wa kina kuhusiana na shule hiyo bado unaendelea.

Bwana Shariff ameeleza kuwa katika kipindi hicho TAKUKURU ilipokea malalamiko 103, kati ya hayo malalamiko 57 yalihusu vitendo vya rushwa na 46 hayakuhusu vitendo vya rushwa na kesi moja ilifunguliwa mahakamani na kesi moja iliyokuwa mahakamani imeamriwa na Jamhuri kupata ushindi.

Aidha, TAKUKURU ilifanya uchambuzi wa mifumo ya utoaji na usimamizi ya adhabu katika Shule ya Sekondari ya Nyamunga katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya baada ya kupokea malalamiko ya kuwatoza wanafunzi wanaokamatwa na simu shilingi 200,000.

Bwana Shariff ameeleza kuwa katika kipindi hicho pia TAKUKURU imefanya uelimishaji umma kupitia klabu za wapinga rushwa 30 kutoka shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati, mikutano ya hadhara 31 na semina 20.  

 Kwa mujibu wa Bwana Shariff, mkazo uliwekwa katika uzuiaji wa vitendo vya rushwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, utoaji wa huduma na kuwashirikisha wadau katika mapambano dhidi ya rushwa na jumla ya wananchi waliopatiwa elimu kuhusu rushwa katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara ni 6,220.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa