• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Rafiki yatambulishwa Mara

Posted on: January 27th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee leo ameipokea rasmi Programu ya TAKUKURU Rafiki kutoka kwa Kamanda wa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara Bwana Hassan Mossi kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Programu hiyo, Mheshimiwa Mzee ameitaka TAKUKURU kuendelea kufuatilia usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mara ili wananchi waweze kupata manufaa yaliyokusudiwa kutokana na miradi hiyo.

“Ninatamani kuona miradi ya maendeleo inayosuasua ikikamilika kwa wakati  ili wananchi waweze kupata manufaa inayotokana na miradi hiyo na ninyi (TAKUKURU) mkifuatilia tutapata matokeo mazuri zaidi” alisema Mheshimiwa Mzee.   

Aidha, Mheshimiwa Mzee ameeleza kuangalia uwezekano wa kuchukua hatua kwa haraka kwa makosa ya uharifu ambayo yapo wazi ili kuleta matumaini kuhusu nia ya Serikali ya kukomesha matukio ya uhalifu.

Mheshimiwa Mzee pia ameipongeza kazi nzuri inayofanywa na TAKUKURU Mkoa wa Mara na kuwataka kuendelea hususan katika utoaji wa huduma kwa wananchi wa vijijini na wasio na uwezo wa kulipia gharama za huduma.

Akizungumza wakati wa kuitambulisha Programu hiyo, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Mara Bwana Hassan Mossi amesema TAKUKURU Rafiki inalenga kuongeza ushiriki wa wananchi na wadau katika kukabili tatizo la rushwa katika utoaji wa huduma kwa jamii na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Bwana Mossi ameeleza kuwa kuanzia sasa, Maafisa wa TAKUKURU watatembelea maeneo mbalimbali katika Wilaya na Halmashauri zote za Mkoa wa Mara ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ushiriki wao katika kupambana na rushwa.

“Tutafanya vikao vingi hadi ngazi ya kata vya kutambua kero zinazowakabili wananchi kwenye utoaji na upokeaji wa huduma za afya, elimu na utekelezaji wa miradi ya maendeleo wa miundombinu ya kutolea huduma” alisema Bwana Mossi.

Bwana Mossi amesema Programu hii inatarajiwa kusaidia kukuza utawala bora kwa kuzuia vitendo vya rushwa visitokee katika utoaji wa huduma kwa umma na katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

TAKUKURU Rafiki ni programu inayotekelezwa kupitia Mpango Mkakati wa TAKUKURU kuanzia mwaka 2022/2023 hadi 2025/2026 na inalenga kupanua wigo wa kushirikisha wananchi na wadau katika kutambua na kutatua kero katika utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa