• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU kuwachukulia hatua waliofuja milioni 90 Tarime

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara kuchunguza na kuwachukulia hatu wote waliohusika katika ujenzi wa bwalo la chakula katika Shule ya Sekondari Manga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 12 Agosti 2021 wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

“Yoyote atakayekuwa amehusika kwa namna moja au nyingine katika hasara hii ya fedha za wananchi achukuliwe hatua za  kisheria na mhakikishe kuwa fedha hizi zinarudi na wanafunzi wanapata bwalo haraka iwezekanavyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo baada ya kushuhudia kuta za bwalo la chakula zikiwa zimepinda na kuezuliwa baada ya jengo hilo kujengwa kwa kutumia nondo za milimita 12 badala ya milimita 16 iliyokadiliwa kwenye BOQ.

Akiwa shuleni hapo Mheshimiwa Hapi amekagua ujenzi wa madarasa na kukemea utaratibu wa kutumia mirango ya mabati kwenye vyumba vya madarasa na nyumba za watumishi badala ya milango ya mbao ambayo ni salama zaidi. 

Mheshimiwa Hapi ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kujenga vyoo vya wanafunzi ndani ya miezi sita ili kuwapunguzia adha wanafunzi wanaokaa bweni kutumia matundu machache ya vyoo ukilinganisha na idadi ya wanafunzi waliopo.

Mkuu wa Mkoa pia akiwa shuleni hapo ameivuja Kamati ya Shule ya Sekondari ya Manga kutokana na usimamizi mbovu wa bwalo hilo na kuisababishia serikali hasara.

Mheshimiwa Hapi akiwa shuleni hapo ameonyeshwa bweni moja lililojengwa kwa nguvu za wananchi miaka 17 iliyopita na Halmashauri imeshindwa kukamilisha ujenzi huo na kuagiza jengo hilo likamilishwe ndani ya miezi sita.

Awali akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Shule hiyo Bi. Editha Nakei ameeleza kuwa ujenzi wa bwalo hilo umetumia zaidi ya shilingi milioni 96 na ulitekelezwa kwa mfumo wa force account.

Bi. Nakei ameeleza kuwa awali fundi aliyekuwa anajenga jengo hilo alisimamishwa lakini walipokea maelekezo kutoka Halmashauri kuwa fundi aendelee na kazi ya ujenzi.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa ameambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye na viongozi wengine wa chama na serikali.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa