• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAKUKURU Kuchunguza miradi ya CSR Tarime

Posted on: August 11th, 2021

TAKUKURU KUCHUNGUZA MIRADI YA CSR TARIME

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mara kuchunguza miradi inayotekelezwa kutokana na fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) zinazotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara katika vijiji 11 vinaouzunguka mgodi huo.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 11 Agosti 2021 wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

“Yoyote atakayekuwa amehusika kwa namna moja au nyingine katika ufujaji wa fedha za wananchi achukuliwe hatua za kisheria mara moja, awe amehama, awe amestaafu au awe amefukuzwa waitwe kujibu mashtaka yao” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ametoa maagizo hayo baada ya kutembelea miradi mine inayotekelezwa kwa kutumia fedha za CSR na kukuta matumizi mabaya fedha, miradi kutekelezwa chini ya kiwango na kutokukamilika kwa muda mrefu pamoja na fedha ya mradi kutolewa na mgodi mapema.

Miradi hiyo ni ujenzi wa Shule ya Msingi Tarajali ya Ntimaro ambapo yamejengwa madarasa sita na kila darasa limegharimu shilingi milioni 26 huku likiwa halijawekewa vigae, umeme, dari halijafungwa gypsum, viti, meza na limeanza kupasuka kabla ya kutumika.

Aidha katika shule hiyo zimejengwa nyumba mbili za walimu zenye uwezo wa kuchukua familia mbili kila mmoja kwa gharama ya shilingi milioni 77 kila nyumba mmoja.

“Matumizi haya ni makubwa mmno na yamepitiliza viwango ambavyo kwa mawaida tunatekeleza miradi ya serikali lakini ubora wa kazi hii pia ni wa hovyo hovyo tu haijafanyika vizuri” alisema Mheshimiwa Hapi.

Katika mradi wa ujenzi wa maabara ya Kituo cha Afya cha Nyangoto, maabara hiyo imejengwa kwa gharama ya shilingi 110 na tangu mwaka 2019 mpaka sasa bado haujakamilika. Aidha katika utekelezaji wa mradi huu, matofali yalinunuliwa mara mbili ya mahitaji yake na hivyo mengi yamebakia huku yakinunuliwa kwa shilingi 2,500 kwa tofali tofauti na bei ya soko.

Katika mradi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa vya shule ya Sekondari ya Matongo, ujenzi huo umegharimu shilingi milioni 80 na umekamilika lakini madarasa hayatumiki kwa sababu hayana viti na meza wakati nondo 900 kati ya nondo zilizonunuliwa kujenga mradi huo zimebakia bila matumizi.

Aidha katika mradi wa ujenzi wa barabara wanannchi wamelalamikia ubora wa barabara hiyo lakini Meneja wa Mamlaka za vijijini na Mijini (TARURA) ameeleza kuwa barabara hiyo imejengwa kwa mujibu wa viwango vinavyohitajika. 

Mhehsimiwa Hapi amewakumbusha watumishi wote wa serikali kutimiza majukumu yao kwa weredi maana serikali imelipa madeni, kuongeza watumishi, kupunguza kodi na kuwapandisha madaraja; watumishi nao wapandishe madaraja ya utendaji wao.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi ameambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samweli Kiboye maarufu kama Namba Tatu, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Diaz Ndomba, viongozi na watendaji wa Wilaya ya Tarime na baadhi ya taasisi za serikali za Mkoa wa Mara.

Ziara ya Mheshimiwa Hapi ilianza tarehe 9 Agosti 2021 ambapo alitembelea wilaya ya Serengeti kwa siku mbili na leo ameanza ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa siku mbili na baada ya hapo ataendelea na ziara yake katika Hamashauri ya Mji wa Tarime.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa