• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Simbachawene kufanya ziara Mkoa wa Mara

Posted on: October 1st, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Boniface Simbachawene leo anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku nne katika Mkoa wa Mara ambapo atakagua na kutembelea miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.

Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, baada ya kupokelewa Mhe. Simbachawene anategemewa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, kuzindua vyumba 13 vya madarasa, matundu 17 ya vyoo na mabweni matano katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songe, kuzindua daraja katika Mtaa wa Majengo Mapya kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Sekondari Mara, Manispaa ya Musoma.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa kesho Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, kuzindua Shule ya Sekondari ya Ingri na kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Utegi Wilaya ya Rorya.  

Msafara utaelekea Wilaya ya Tarime, ambapo Mhe. Simbachawene atazindua Shule ya Msingi Komote na mradi wa maji Kemakorere na baadaye kufanya mkutano wa hadhara katika eneo la Kemakorere.

Tarehe 3 Oktoba, 2024 Mhe. Simbachawene anategemea kuzindua Zahanati ya Getarungu na kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Getarungu, kuweka jiwe la msingi katika barabara ya Stendi Mpya katika mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti.

Baada ya hapo msafara unatarajiwa kuelekea Wilaya ya Butiama ambapo Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuzindua Shule ya Msingi ya chifu Manyori na kufanya mkutano wa hadhara katika stendi ya mabasi katika eneo la Nyamisisi.

Tarehe 4 Oktoba, 2024 Mhe. Simbachawene anatarajiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Zahanati ya Nambaza, kutembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara na kuzindua Shule ya Sekondari ya Bunda Mjini kabla ya kuhitimisha ziara hiyo na mkutano wa hadhara katika eneo la Stendi ya Zamani iliyopo katika Mji wa Bunda.

Mhe. Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, lililopo katika Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma katika ziara hii anatarajiwa pia kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hapa nchini tarehe 27 Novemba, 2024.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa