• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Shule bora yatoa mafunzo ufundishaji kiingereza

Posted on: December 19th, 2023

Walimu Wakuu na Maafisa Elimu Kata ambao shule zao zilifanya vibaya kwenye Somo la Kiingereza katika mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba mwaka 2023 Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti leo tarehe 27 Novemba, 2023 wamepewa mafunzo ya namna ya kusimamia ufundishaji wa somo hilo yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Azimio A. 

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Mujibu Mustafa Babara ameeleza kuwa mafunzo hayo ni muhimu na kuwataka washiriki wa mafunzo kufuatilia mafunzo hayo ili kwenda kubadilisha hali ya ufundishaji wa somo hilo.

“Tunataka mkimaliza mafunzo hayo, mabadiliko ya wazi yaonekani kwa namna walimu wenu watakavyokuwa wanafundisha na namna wanafunzi watakavyoongeza ufaulu wa asomo la kiingereza katika shule zenu” amesema Bwana Babara.

Bwana Babara ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara wataalamu hao watakuwa wakwanza kupewa mafunzo ya kusimamia na kutekeleza muhutasari wa somo la Kiingereza kwa shule za Msingi kulingana na Mtaala wa Elimu ya Msingi, 2023.

“Ninyi mnapewa mafunzo kwenye mada mpya kabisa ambayo nina uhakika sio walimu wote hapa nchini watapata fursa mliyoipata leo, tuyatendee haki haya mafunzo na tukawajibike katika kuwasimamia walimu wanaofundisha” amesema Bwana Babara.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Bwana Sam Mwita ameeleza kuwa ufaulu wa somo la Kiingereza kitaifa ni asilimia 34 na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ilikuwa ni ya mwisho katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba, 2023.

“Ni mategemeo yetu kuwa mafunzo haya, na mafunzo yatakayotolewa kwa waliu kesho yataboresha ufundishaji wa wanafunzi na hivyo kuja kuboresha matokeo ya somo la kiingereza katika mitihani ya ndani na mitihani ya Taifa” amesema Bwana Mwita.

Bwana Mwita ameelezea imani yake kuwa walimu hao wanaouwezo wa kufanya mabadiliko na wanasifa za kufanya mabadiliko na kuwataka kutekeleza kwa ufanisi mpangokazi watakaotoka nao katika mafunzo hayo.

Kwa upande wake, Mdhibiti Ubora wa Kanda ya Ziwa Bibi Lucy Nyanda ameeleza kuwa kuna mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu na hivyo walimu hawana budi kujifunza kuhusu mtaala na sera mpya za elimu zilizoanza kutumika hivi karibuni.

Bibi Nyanda amewataka washiriki hao kuchukulia mafunzo hayo kama chachu ya kujifunza mambo yote yanayohusiana na elimu na mabadiliko ya mitaala na sera ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mafunzo ya Wakuu wa Shule na Maafisa Elimu Kata yanatarajiwa kufuatiwa na mafunzo kwa walimu wanaofundisha somo la Kiingereza katika shule hizo yanayotarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 28 Novemba, 2023.

 Mafunzo haya yanatolewa na Wakala wa Maendeleo ya Elimu (ADEM) na kufadhiliwa na Mradi wa Shule Bora.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa