• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Shirikianeni na viongozi kutatua kero- Mzee

Posted on: January 30th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee leo amezungumza na viongozi wa wananchi wa eneo la Ghuba ya Speke, katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda na kuwataka wananchi kuwashirikisha viongozi wa Serikali changamoto zao ili waweze kusaidiana kuzitatua.

Mheshimiwa Mungiya ameeleza hayo wakati akizungumza na viongozi wa wananchi wa Kata ya Nyatwali  katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo ofisini kwa Mkuu wa Mkoa na kumuomba awasaidie ili wanapoondoka katika eneo la Ghuba ya Speke wapate fidia wanazostahili na na walipwe mapema ili waweze kuendelea na majukumu yao mengine.

 “Sisi viongozi tupo hapa kwa ajili yenu, tukishirikiana mambo yote yaawezekana ikiwa ni pamoja na mambo magumu ambayo tunaweza kudhani hayawezekani lakini tukiweka nguvu zetu kwa pamoja yote yanawezekana” amesema Mheshimiwa Mzee.

Aidha, Mheshimiwa Mzee amewashukuru viongozi hao kuja kuzungumza nae na kuwataka kuwasiliana nae kama kuna changamoto nyingine yoyote itakayowapata wakati wa utekelezaji wa utwaaji wa eneo la Nyatwali.

Mheshimiwa Mzee amewataka viongozi hao kuwaelimisha wananchi wa Nyatwali kuhusiana na umuhimu wa wao kushirikiana na wathamini wakati wa kufanya uthamini wa maeneo na mali zao ili waweze kulipwa fidia stahiki kwa mujibu wa sheria.

Taarifa ya viongozi hao iliyosainiwa na Diwani wa Kata ya Nyatwali Mheshimiwa Mashimo Malongo kwa niaba ya wananchi wa Nyatwali, imeeleza kuwa wananchi wa Nyatwali wameomba Serikali kutoa nyongeza ya fidia ili wananchi watakaohamishwa waweze kujikimu baada ya kuhamisha kwa hiari katika eneo hilo.

“Wananchi wa Kata ya Nyatwali hawapingani na Serikali na wala hawakatai kuhama lakini wanamashaka juu ya fidia watakayolipwa ili kupisha uendelezaji wa eneo hilo” na kuongeza kuwa kufuatia ziara ya Mawaziri wa Kisekta katika eneo hilo, wananchi wamehamasika kuchukua fomu za utambuzi na kuthaminishwa kwa ardhi na mali wanazomiliki.

Wakizungumza na Mkuu wa Mkoa, viongozi hao wameiomba Serikali kuwalipa fidia ya ardhi sawa na bei ya ardhi inayouzwa na Halmashauri ya Mji wa Bunda ambako wengi wao wataenda kununua maeneo baada ya kuhamisha kutoka katika Kata ya Nyatwali. 

Mapendekezo mengine ni pamoja na Serikali kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu ukokotoaji wa majengo; wameomba nyongeza ya malipo ya makaburi kukidhi gharama halisi za kuhamisha makaburi; nyongeza ya fidia za mazao ya chakula, mazao ya biashara na miti; fidia za mali zisizohamishika; wapewe fidia ya usumbufu (Disturbance allowance); gharama za kuanzia makazi; fidia ya kusafirisha mifugo; fidia ya vyoo; na fidia ya vyombo vya uvuvi.

Viongozi hao wameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali katika kuhakikisha utwaaji wa eneo hilo unafanyika kwa amani na utulivu wakati wote wa zoezi la uthamini, ulipaji wa fidia na uhamaji wa wananchi.

Viongozi waliokutana na Mkuu wa Mkoa wa Mara ni pamoja na Diwani wa Kata ya Nyatwali, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Kata ya Nyatwali, Wenyeviti wa Mitaa ya  Tamau, Serengeti, Nyatwali na Kariakooo na wananchi wanne waliowawakilisha wenzao kutoka katika mitaa ya Kata ya Nyatwali.

 Serikali imeamua kulitwaa eneo la Ghuba ya Speke, katika Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda kwa ajili ya uhifadhi endelevu wa ikolojia ya Hifadhi ya Taifa ya Serengati na kulinda usalama wa wananchi wa eneo hilo ambalo lipo kandokando ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Ziwa Victoria.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa