• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali yatoa vifaa vya Maabara kwa Sekondari 1258 nchini

Posted on: April 27th, 2020

Serikali imetoa vifaa vya maabara vya masomo ya Kemia, Fisikia na Biolojia kwa shule za sekondari 1258 hapa nchini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tano ili kuinua kiwango cha elimu hususani masomo ya sayansi hapa nchini.

Akizungumza leo tarehe 20 Aprili 2020 wakati wa kukagua vifaa vya maabara vilivyoletwa katika Shule ya Sekondari ya Kebogwe iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema tayari vifaa hivyo vimeshasambazwa na kuanza kutumika katika shule mbalimbali hapa nchini.

“Huu ni uwekezaji mkubwa sana kwa serikali katika sekta ya elimu, na lengo ni kuinua ufundishaji wa masomo ya sayansi kwa wanafunzi wa sekondari hapa nchini” alisema Eng. Nyamhanga.

Eng. Nyamhanga ameeleza kuwa katika bajeti ya mwaka 2020/2021 iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni, TAMISEMI imepanga kutoa fedha za ujenzi wa maabara saba za sayansi kwa kila halmashauri hapa nchini ili kuendeleza jitihada za kuinua ufundishaji wa masomo ya sayansi. 

Wakati huo huo, Eng. Nyamhanga ameahidi kuwa TAMISEMI itatoa fedha za kukamilisha ujenzi wa Jengo la Utawala na nyumba ya walimu katika Shule ya Sekondari ya Kebogwe.

Akizungumza baada ya kukagua shule hiyo na kupokea taarifa ya shule, Eng. Nyamhanga amesema “serikali itaunga mkono juhudi za wananchi ambao wamejenga majengo hayo na wameshindwa kuyamalizia”.

Aidha ameipongeza shule hiyo kwa kuendelea kuboresha taaluma ingawa bado ina changamoto ni nyingi ikiwemo za miundombinu ya kujifunzia na kufundishia na nyumba za walimu.  

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Sekondari ya Kebogwe ameeleza kuwa shule hiyo ilianza mwaka 2015 kwa kujengwa kwa nguvu za wananchi. Mpaka wakati huu shule ina jumla ya wanafunzi 333 wa kidato cha kwanza hadi cha nne.

 Ameeleza kuwa idadi ya wanafunzi imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Shule ilianza ikiwa na wanafunzi 37 wa kidato cha Kwanza lakini mpaka sasa, shule ina wanafunzi 104 wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2020.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa