• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali yataifisha kilo 27.5 ya dhahabu

Posted on: June 16th, 2020

Serikali imetaifisha kilo 27.5 za madini ya dhahabu yenye thamani ya shilingi bilioni 3 pamoja na gari aina ya Toyota Harrier mali ya Bwana Barwesh Gandecha Mkazi wa Jiji la Mwanza yaliyokamatwa katika eneo la Sirari katika Wilaya ya Tarime, Mkoani Mara.  

Akizungumaza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini ambaye pia ni Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Bwana  Biswalo E. K. Maganga  ameeleza kuwa mbali na kutaifisha mali hizo, Bwana Gandecha pia amehukumiwa  kulipa faini ya shilingi milioni 315.

“Hukumu hiyo imetolewa jana tarehe 15 Juni 2020 na Hakimu Veronica Mgendi wa mahakama ya Wilaya ya Tarime baada ya Bwana Gadencha kufikishwa mahakamani  na kukiri makosa ya utakatishaji wa fedha na umiliki wa madini kinyume cha sheria” alisema Bwana Maganga.

Ameeleza kuwa Bwana Gandecha alikamatwa katika mji wa Sirari Mei 15, 2020 akiwa na dhahabu hiyo ambayo awali alidanganya kuwa aliingiza nchini ikitokea nchi jirani ya Kenya lakini hakuwa na nyaraka za kuonyesha kuwa madini hayo yalitokea nchini Kenya.

Bwana Maganga ameeleza kuwa uchunguzi umebaini kuwa dhahabu hiyo imepatikana kupitia mtandao haramu unaofadhiliwa na Bwana Gandecha na kuwa alijaribu kutafuta nyaraka kwa njia ya udanganyifu ili kuweza kuhalalisha umiliki wa madini hayo.

“Uchunguzi pia umebaini kuwepo kwa watumishi wa serikali katika taasisi za umma ambao walikuwa wanamsaidia Bwana Gadecha kutengeneza nyaraka za kuhalalisha umiliki wa madini hayo na taratibu za kisheria zinafuatwa juu ya watumishi hao waliohusika” alisema Bwana Maganga.

Kwa mujibu wa Bwana Maganga serikali imetaifisha jumla ya kilo 425 za dhahabu katika kipindi cha miaka mitano tangu serikali ianze kutaifisha madini yanayomilikiwa kinyume cha sheria.

Akizungumza katika kikao hicho kati ya DPP na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mara, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameeleza kuwa mtu huyo alikamatwa na vyombo vya dola kutokana na ushirikiano mzuri uliopo baina ya vyombo hivi katika Mkoa wa Mara na wananchi ambao waliamua kutoa taarifa juu ya umiliki wa madini hayo bila kufuata sheria.

“Ninawashukuru sana kwa ushirikiano huu na niwaombe wote wanaotaka kufanya biashara ya madini katika Mkoa wa Mara kufuata sheria na taratibu ili mfanye biashara yenu kihalali bila kubughudhiwa na mtu” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa ufanyaji wa biashara ya madini kwa njia halali utawasaidia wafanyabiashara kufanya biashara zao kwa tija na kuwapatia maendeleo endelevu ambayo yatawanufaisha watanzania wote ambayo ndio nia ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa