• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali kuubadilisha Musoma kuwa Mji wa Utalii

Posted on: September 11th, 2020

Uwekezaji katika upanuzi na uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Musoma unaofanywa na serikali ya unalenga kuubadilisha mji wa Musoma kuwa mji wa Utalii na Mkoa wa Mara kuwa ndio lango kuu la kuingilia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 11 Septemba 2020.

“Uwanja wa ndege wa Musoma utakapokamilika utaleta ndege za Shirika la Ndege la Tanzania na ndege nyingine ambazo zitaleta watalii kwa wingi hususan katika msimu wa watalii” alisema Mheshimiwa Malima.

Amewahamasisha wafanyabiashara kuwekeza zaidi katika huduma za kuwahudumia watalii ili uwanja utakapokamilika kuwe na huduma za kuwapa watalii.

Amezitaja huduma hizo kuwa ni pamoja na chakula, mahoteli, mabenki, hospitali, usafiri, na kadhalika ambazo zitawafanya watalii kufurahia kuwepo Tanzania na hivyo kutamani kurudi tena.

Aidha amewataka wakazi wa Mkoa wa Mara kubadilisha mtazamo wao na kuanzisha ukarimu kwa wageni ili waweze kufaidika na fursa za utalii zilizomo katika Mkoa wa Mara.

“Mara ndio sehemu pekee ambapo Serengeti inakutana na Ziwa Victoria, wanyama wanapovukia kwenda Masai Mara, Kenya, Nyumbu wanapozaliana na kadhalika, tukiendelea na tabia zetu mbaya zitawatisha watalii na tutabakia kuwa nyuma kimaendeleo” alisema Malima.

Aidha amehimiza uwekezaji katika miji mingine ya Mugumu, Bunda na Natta ili kuweza kuwapokea na kuwahudumia watalii wanaotegemewa kuja baada ya uwanja wa ndege kukamilika Musoma.

Mheshimiwa Malima alisema Rais ametoa ahadi ya kukamilisha uwanja huo kutokana na umuhimu wake kwa Mkoa wa Mara lakini pia kwa ukuaji wa sekta ya utalii hapa nchini.

Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli alitoa ahadi ya kukamilisha uwanja wa ndege wa Musoma tarehe 5 Septemba 2020 katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mukendo katika Manispaa ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa