• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali kukamilisha malipo ya fidia Nyatwali

Posted on: April 22nd, 2025

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeiagiza Serikali kutoa malipo ya asilimia 10 iliyobakia ya fidia ya wananchi wa mitaa minne ya Kata ya Nyatwali, Wilaya ya Bunda wanaohama kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Akizungumza wakati wa kuwasalimia Mji wa Bunda, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amemuagiza Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba kukamilisha malipo ya fidia ya asilimia 10 iliyobakia mapema iwezekanavyo.

“Nilizungumza na Mhe. Rais kuhusu malipo ya fidia ya Nyatwali na ameridhia fedha hizo zilipwe na mpaka sasa tayari asilimia 90 ya malipo ya fidia yameshalipwa imebakia asilimia 10 tu ya fidia hizo” amesema Mhe. Nchimbi.

Aidha, Balozi Nchimbi amewataka wananchi wenye malalamiko kuhusiana na fidia ya Nyatwali iliyotolewa kuyawasilisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara ili yaweze kushughulikiwa na Serikali.

Mhe. Nchimbi amewataka wananchi wa Bunda kutulia na kutoa malalamiko yao kwa ustaarabu wakati Serikali inaendelea kukamilisha malipo ya fidia hiyo na kuwahakikishia kuwa kwa namna anavyomfahamu Waziri wa Fedha fidia hiyo italipwa hivi karibuni.

Wakati huo huo, Mhe. Nchimbi amewataka wananchi kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu na kuacha kuwasikiliza viongozi wanaohubiri uvunjifu wa amani na vurugu katika uchaguzi huo.

“Awamu ya pili ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura karibu utafika kwa awamu ya pili, kwa wale wote wanaohitaji kuboresha taarifa tutumie fursa hiyo kuboresha taarifa ili kuweza kushiriki uchaguzi” amesema Mhe. Nchimbi.

Mhe. Nchimbi amesema kutokana na uchaguzi mkuu kumekuwepo na vichocheo vya vurugu, uhasama na matukio ya uvunjifu wa amani na kuwataka wananchi wasikubali kuharibu amani iliyopo ambayo imedumu kwa muda mrefu na kujihadhari na matukio hayo kwani kuna maisha baada ya uchaguzi   

Mhe. Nchimbi ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi kukipigia kura Chama cha Mapinduzi kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya CCM yam waka 2020-2025 hapa nchini.

Mhe. Nchimbi leo ameanza ziara ya siku tano katika Mkoa wa Mara ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar wenye kauli mbiu “Muungano wetu ni Dhamana, Heshima na Tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”.

Mapokezi hayo yamehudhuriwa na viongozi wa CCM Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Bunda, watendaji wa umma, wanachama wa CCM na wananchi wa Wilaya ya Bunda na maeneo jirani.

 Kesho ziara inaendelea katika Wilaya ya Musoma ambapo atakagua maendeleo ya ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa Ndege Musoma, kukagua maendeleo ya ujenzi katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, atatembelea Ofisi za CCM Mkoa wa Mara  kukagua ukumbi wa mikutano wa CCM na kufanya kikao cha ndani na Halmashauri Kuu iliyoboreshwa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa