• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali ipo tayari kutoa fidia Nyatwali

Posted on: June 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Mji wa Bunda katika uwanja wa stendi ya zamani na kuwahakikishia wananchi wa Kata ya Nyatwali kuwa malipo ya fidia yataanza kutolewa muda wowote kuanzia wiki ijayo.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa malipo yapo tayari na kuwataka wananchi kujiandaa kupokea fidia zao na kuhama katika eneo hilo kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

“Malipo ya fidia ya Nyatwali yameshatoka na mimi ninategemea muda wowote kuanzia wiki ijayo Serikali kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) litaanza kutoa fedha hiyo kwa wananchi wa eneo la Nyatwali” amesema Mhe. Mtambi.

Kanali Mtambi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kutenga maeneo maalum ambayo watauziwa wananchi watakaohama kutoka katika Kata ya Nyatwali kwa bei nafuu ili kuwasaidia watakaotaka kubaki ndani ya Wilaya ya Bunda kupata maeneo kwa haraka.  

Mhe. Mtambi amewaelekeza Wakurugenzi hao kuitisha vikao maalum vya Mabaraza ya Madiwani kujadili suala la kutenga maeneo na kuwauzia wananchi hao wiki ijayo na kuagiza ofisi yake ipate taarifa ya utekelezaji wa maagizo hayo haraka iwezekanavyo.

Aidha, Mhe. Mtambi amewasistiza wananchi wa Nyatwali watakaolipwa fidia hizo kutumia fedha hizo kwa ajili ya kufanyia shughuli za maendeleo yao na familia zao.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara ameiagiza Halmashauri ya Mji wa Bunda kumkabidhi fidia ya  viwanja viwili Bibi Monica Palapala, mkazi wa Bunda Stoo hadi kufikia Jumatatu tarehe 1 Julai, 2024 ili kufidia eneo lake lililochukuliwa na barabara baada ya kupima eneo hilo.

Mhe. Mtambi ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko ya Bibi Palapala ambaye alikuwa na shamba lake eneo la Bunda Stoo na baadhi ya eneo lake kupitiwa na barabara na kubakiwa na kiwanja kimoja badala ya viwanja vitatu alivyopimiwa awali.

aidha, Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuzingatia usafi kwenye makazi na biashara zao ili kuweza kuwavutia wawekezaji na watalii wanaoingia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupumzika katika Mji wa Bunda.

Kanali Mtambi pia amewataka vijana kuunda vikundi vya uzalishaji mali ambavyo vinaweza kusaidiwa mikopo au ujuzi na wataalamu wa Serikali na wadau wengine waliopo katika Mkoa wa Mara ili kuweza kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake, Bwana Peter Alphonce Chacha mkazi wa Mtaa wa Tamau, Kata ya Nyatwali ameipongeza Serikali kwa kulipa fidia wananchi wa eneo hilo, kwa sasa changamoto ni nyingi maana hawaruhusiwi kuliendeleza eneo hilo baada ya kufanyiwa tathmini.

Bwana Chacha amesema walikuwa wanaishi hapo kwa wasiwasi kwa kuwa walikuwa wanavamiwa na wanyama mara kwa mara kutoka SENAPA na japokuwa walikuwa wanalipwa fidia lakini ilikuwa haitoshi ikilinganishwa na mazao waliyokuwa wanapoteza.

Kwa upande wake, Bwana Ibrahim Gigita Joseph mkazi wa Mtaa wa Kariakoo, Kata ya Nyatwali amesema kwa muda wa miaka miwili tangu wafanyiwe tathmini kwa ajili ya kulipwa fidia walikuwa wanaishi kama kifungoni.

“Bora tulipwe tukaanzishe maisha mapya sehemu nyingine, tuwe huru na labda watoto wetu watakuja kupata kazi katika hifadhi hii hapo baadaye” amesema Bwana Joseph.

Mkutano huo umehudhuriwa na baadhi ya Maafisa kutoka Sektretarieti ya Mkoa wa Mara, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Bunda, Wenyeviti wa Halmashauri , Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Halmashauri za Mji wa Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa