• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali inaendelea na uchunguzi wa mtu kupotea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti

Posted on: December 17th, 2020

Serikali mkoani Mara inaendelea kufanya uchunguzi wa tukio la kupotea kwa Bwana Mango Kahuru (20) mkazi wa kijiji cha Kenyamosabi katika Wilaya ya Tarime wakati akichunga ng’ombe ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) tarehe 11 Desemba 2020.

Akizungumza na wananchi wa Kata za Kwishancha, Gorong’a na Nyanungu katika Shule ya Msingi Kinyamosabi leo tarehe 16 Desemba 2020, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amesema vyombo vya ulinzi na usalama vya Mkoa na Wilaya ya Tarime vinaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

“Kwa sasa bado uchunguzi  unaendelea na tayari Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Tarime imetembelea eneo la tukio lililopo ndani ya hifadhi na kujionea hali halisi ya sehemu tukio lilipotokea” alisema Mheshimiwa Malima.

Mkuu wa Mkoa pia amewaomba wanafamilia na wananchi wa eneo hilo kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola vinavyoendelea kufanya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo ili uchunguzi uweze kukamilika kwa haraka na majibu yaweze kupatikana kutokana na tukio hilo.

Hata hivyo Mheshimiwa Malima amewaasa wananchi wa eneo hilo kuacha mara moja kupotosha ukweli juu ya tukio la kupotea kwa Bwana Kahuru kwani hamna mwenye uthibitisho wa taarifa mbalimbali za upotoshaji zinazosambazwa kuhusiana na tukio hilo.

“Tangu tukio hili limetokea kuna maneno mengi sana yametokea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na tukio hili na ukiyaangalia maneno mengi ni ya uongo na uzushi, sasa ndugu zangu sheria zipo zinafanyakazi, tuache upotoshaji hausaidii wakati huu ambapo bado tunaendelea kumtafuta kijana wetu” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima amewaomba wananchi wa eneo hilo kuishi kwa amani na kuendelea na shughuli zao za maendeleo wakati huu ambapo vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Aidha Mheshimiwa Malima amewaonya wananchi wa eneo hilo kuacha mara moja tabia ya kuanzisha migogoro isiyoisha katika eneo hilo ambapo tangu yeye awe Mkuu wa Mkoa huo miaka mitatu iliyopita ameshatatua migogoro mingi sana ikiwemo migogoro ya mipaka kati ya wananchi wa eneo hilo na SENAPA.

“Kwa Mkoa wa Mara, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti inapakana na Wilaya za Serengeti, Butiama na Tarime, lakini pamoja na ukweli kuwa Tarime mnaeneo dogo zaidi la mpaka, lakini mmekuwa na migogoro mingi sana ukilinganisha na wilaya za Bunda na Serengeti ambazo mipaka yake ni mikubwa zaidi “ alisema Mhehsimiwa Malima.

Aidha Mheshimiwa Malima amewatahadharisha wananchi wa eneo hilo kuacha tabia ya kuingia hifadhini na kufunga waya za mitego na kuua wanyama pori ndani ya hifadhi pamoja na kufanya shuguli nyingine za kibinadamu.

“Hivi karibuni mmefunga mitego na mmeua zaidi ya wanyama 100 kwa wakati mmoja na mkawaacha hapo hapo wala hamkuchukua hizo nyama zote, huu ni uharibifu na ni kinyume cha sheria” alisema Mheshimiwa Malima.     

 “Kama kuna mtu yoyote anayewahamasisha kwenda kufanya uharibifu katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti anawaongopea, serikali ipo kazini na taarifa zenu za kutega mitego kwa ajili ya wanyama tunazo na tunazifanyia kazi” alisema Mheshimiwa Malima. 

Aidha aliwaagiza SENAPA kuendelea kutoa elimu kwa umma na kuimarisha ujirani mwema katika vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo ili kupunguza baadhi ya migogoro na wananchi hao kutokana na kukosa uelewa kuhusu sheria na namna wanavyonufaika na uwepo wa hifadhi hiyo.

Mheshimiwa Malima pia aliwataka viongozi wa vijiji hivyo kutoa taarifa za matukio mbalimbali yanapotokea kwenye vyombo la ulinzi na usalama, ofisi ya Mkuu wa Wilaya na ofisi yake ili malalamiko yao yaweze kupatiwa ufumbuzi kwa haraka zaidi na sio kusubiri viongozi wanapotembelea maeneo hayo.

Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa ambaye aliambatana na Kamati za Ulinzi na Usalama, maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), SENAPA na watumishi wa serikali, alipokea maelezo na maoni ya familia, wananchi na viongozi waliokuwepo katika eneo hilo.  

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Kenyamusabi Bwana Mwita Raphael Salima ameeleza kuwa katika miaka ya 2019 na 2020 watu watatu wanasadikiwa kuuawa na askari wa SENAPA na wengine kujeruhiwa baada ya kuingia katika hifadhi hiyo.

Aliwataja wanaosadikiwa kuuawa kuwa ni Matiko Kebohi Marwa, Mwita Mwita Sereka na Manga Kahuru Manga ambaye amepotea akiwa anachunga ng’ombe katika hifadhi hiyo na mpaka sasa hajulikani alipo.

“Aidha askari wamewajeruhi Marwa Masambe, Marwa Mwita Matutu na Bwana Marwa Chacha Wambura ambaye mpaka sasa amepata ulemavu wa kudumu” alisema Bwana Salima.

Aidha Bwana Salima aliomba SENAPA kuimarisha uhusiano na vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo kama ilivyokuwa hapo awali ili wananchi waweze kupata elimu ya uhifadhi na kusaidiaa katika kuilinda Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa