• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali imetenga bilioni 1.3 kujenga Uwanja wa Ndege Serengeti

Posted on: February 27th, 2025

7Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA) imetiliana saini na Kampuni ya Saba Engineering kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Serengeti katika Halmashauri ya Serengeti, Mkoa wa Mara tarehe 27 Februari, 2025.

Akizungumza katika hafla ya kutia saini mkataba huo, Mkurugenzi Mkuu wa TAA Bwana Abdul Mambokaleo amesema Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uwanja huo katika mwaka wa fedha 2024/2025.

“Kampuni ya Saba Engneering imepewa mkataba wa miezi sita na baada ya kukamilisha upembuzi  yakinifu itatoa ushauri wa kitaalamu wa namna bora ya kujenga uwanja huo” amesema Bwana Mambokaleo.

Bwana Mambokaleo amesema kuwa Serikali inajenga uwanja huo ili kuongeza idadi ya watalii wanaoitembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) pamoja na kurahisisha usafiri wa wananchi na mizigo kuingia katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Dkt. Maulid Suleiman Madeni ameipongeza TAA kwa kuchukua hatua za kutenga fedha na kuanza ujenzi wa uwanja huo na kusema kuwa uwanja huo utaleta mapinduzi ya kiuchumi kwa wananchi wa Serengeti.

“Baada ya uwanja huu kukamilika huu kukamilika watalii wote watashuka moja kwa moja Serengeti na kuingia hifadhini na wakati wa msimu wa utalii tunategemea kupata ndege hadi 100 kwa siku moja” amesema Dkt. Madeni.

Dkt. Madeni amesema uwanja huo utasaidia kuboresha uchumi wa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Mkoa wa Mara kwa ujumla kutokana na kujengwa kwa ofisi mbalimbali katika Mji wa Serengeti kama sehemu ya uwepo wa uwanja huo.

Dkt. Madeni amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuanza kutenga fedha za ujenzi wa uwanja huo.

Uwanja huu unaongeza viwanja vya ndege vya Mkoa wa Mara kuwa viwili baada ya Serikali kutoa bilioni 35 kwa ajili ya upanuzi na ukarabati wa Uwanja wa Ndege Musoma ambao pia unatarajiwa kusaidia kurahisisha usafiri kwa watalii wanaoingia katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa kutumia lango kuu la Ndabaka lililopo Wilaya ya Bunda.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa