• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mtanda azungumza na Wazee wa Musoma

Posted on: June 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amekutana na kufanya mazungumzo na  wazee wa Manispaa ya Musoma katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtanda amewaomba wazee kumpa ushirikiano yeye na viongozi wengine wa Serikali katika kuuongoza Mkoa wa Mara na hususani kwa kutoa maoni, ushauri na mawazo ya namna ya kuujenga Mkoa wa Mara.

“Ninawaomba sana mtupatie ushirikiano katika kutekeleza yale yote tunayotakiwa kuyafanya katika Mkoa wa Mara” alisema Mheshimiwa Mtanda.

Mhe. Mtanda amewaahidi wazee kuwa Ofisi yake itasimamia upatikanaji wa huduma stahiki za wazee na kusimamia udhibiti masuala ya ukatili dhidi ya wazee na watu wengine.

Mheshimiwa Mtanda ameeleza kuwa lengo la kukutana nao ni kujitambulisha kwao ili wampe Baraka zao kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yake katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wananchi wote wa Mkoa wa Mara kuwasilisha kero zao, ushauri na maoni ofisini kwake na ofisi za viongozi wa Serikali ili waweze kuzifanyia kazi.  

Wakati huo huo, Mhe. Mtanda ameziagiza Halmashauri za Mkoa wa Mara kuwafanyia sensa wazee na kutoa vitambulisho vya wazee wanaostahili ili waweze kupata huduma za matibabu bure kwa mujibu wa sheria na kanuni.

Aidha, amezitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa mabaraza ya wazee yanafanyika kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na serikali kuhusu mabaraza ya wazee.

Mheshimiwa Mtanda pia ameongelea wajibu wa jamii na viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya vijiji, mitaa, Kata, Halmashauri na Mkoa katika kuwatunza wazee wanaoishi katika maeneo yao.

kwa upande wao, wazee wa Manispaa ya Musoma wamemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kukutana nao na kumuahidi kumpatia ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake.

Akizungumza katika kikao hicho Bibi Amina Magoti ambaye ni Katibu wa Baraza la Wazee Mkoa wa Mara amesema kikao hicho kimekuja wakati muafaka wakati Mkoa unajiandaa kufanya maadhimisho ya kupinga Ukatili dhidi ya Wazee.  

Aidha, Bibi Amina ameeleza kuwa Mkoa wa Mara una rasilimali nyingi na eneo kubwa la kilimo na kumuomba Mkuu wa Mkoa kutembelea maeneo hayo. 

Aidha, wazee hao wamemuomba Mkuu wa Mkoa na serikali kwa ujumla kufufua viwanda na kujenga viwanda vipya ili watoto wapate ajira.

Wengine walioshiriki katika mazungumzo hayo ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Magiri Benedicto Malegesi , Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Msalika Robert Makungu, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na lishe Dkt. Zabron Masatu, Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. Wiliam Gumbo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma Bwana Bosco Ndunguru.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa