• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mtanda atoa muda Tarime DC kukamilisha miradi

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo tarehe 30 Oktoba, 2023 amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambapo ametoa muda wa kukamilisha miradi ya maendeleo.

Katika ziara hiyo Mhe. Mtanda amekagua ujenzi wa Kituo cha Afya Mtana kinachojengwa na fedha za Serikali Kuu shilingi milioni 550 na Halmashauri shilingi milioni 250 ambapo ujenzi wake unaendelea na baadhi ya majengo yameanza kutoa huduma na kumtaka mkurugenzi kukamilisha mradi huu ndani ya mwezi mmoja.

“Mganga Mkuu wa Halmashauri na Mhandisi hakikisheni mradi huu ndani ya mwezi mmoja unakamilika na Mhe. Diwani ninaomba unipigie picha na kunitumia kama mradi utakuwa umekamilika” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, Mhe. Mtanda amekemea kitendo cha Halmashauri hiyo kuongeza shilingi milioni 250 katika mradi huo ambao sehemu nyingine unatumia shilingi milioni 500 tu hadi kukamilika.

Aidha, Mhe. Mtanda ametembelea Shule ya Sekondari Mtana ambayo inajengwa kupitia mradi wa maendeleo ya elimu ya Sekondari (SEQUIP) katika Kijiji cha Mtana na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kukamilisha mradi huo ndani ya siku 14.

Aidha, amekemea kitendo cha Halmashauri hiyo kukaa na fedha muda mrefu kabla ya kuanza kutekeleza mradi huo jambo ambalo amesema halikubaliki katika Mkoa wa Mara.

Katika ziara hiyo pia ametembelea mradi wa maji eneo la Nyarero na kumtaka Meneja wa RUWASA na Meneja wa TANESCO Wilaya ya Tarime kufunga umeme na kuhakikisha maji yanatoka ndani ya siku 10 ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

Katika kuhitimisha, Mhe. Mtanda alifanya mkutano na wananchi wa kitongoji cha Nyamichere, Kijiji cha Nyikunguru na kuwaasa wananchi kuacha kuvamia Mgodi wa Dhahabu wa North Mara na badala yake kutafuta shughuli nyingine za maendeleo.

Aidha, Mheshimiwa Mtanda alisikiliza kero na maoni ya wananchi na kuahidi kulitafutia ufumbuzi suala la barabara inayoingia katika kijiji hicho ambayo wananchi wamesema ilifungwa na mgodi wa North Mara.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii, watendaji wa Halmashauri na taasisi nyingine za umma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa