• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mtambi kusikiliza kero za wananchi kila Jumanne

Posted on: May 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi leo amezungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kuzungumzia mpango wake wa kuanza kusikiliza kero za wananchi kila siku ya jumanne kuanzia tarehe 01 Juni, 2024.

Akizungumza na watumishi hao, Mhe. Mtambi amesema atafungua kliniki maalum ya kusikiliza kero za wananchi akishirikiana na wataalamu mbalimbali waliopo katika Mkoa wa Mara.

“Huu utakuwa ni utaratibu wa kudumu kwa kila siku ya Jumanne tutasikiliza kero za wananchi ambapo wataalamu watazichakata na kila siku ya Ijumaa tutatoa mrejesho au maamuzi ya kero za wananchi waliosikilizwa wiki hiyo baada ya mimi kujiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema atahakikisha kero zote zitakazoletwa na wananchi zinasikilizwa na viongozi na watendaji wa umma katika maeneo yao ili kuwawezesha wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo kwa amani.

“Tufungue milango ya ofisi za Serikali, tuwasikilize na kutatua changamoto za wananchi na kuwahudumia wananchi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, sheria na taratibu za utumishi wa umma” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi pia amewataka Wakuu wa Wilaya, wakuu wa taasisi za umma, wenyeviti na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Mara kutenga siku ya kusikiliza kero za wananchi na kutatua migogoro yao kwa kuzingatia sheria, busara na maoni ya wananchi wa eneo husika.  

Mhe. Mtambi amewataka watumishi wa Serikali kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa wao ni wawakilishi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye maeneo wanayotolea huduma  na kuongeza kuwa watumishi wanauwezo wa kuwafanya wananchi waipende Serikali yao au waichukie.

Wakati huo huo, Mhe. Mtambi amesikiliza kero za watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kumtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kufuatilia kwa ukaribu suala la kumpandisha cheo Bwana Lameck Chegeni,  Mtendaji wa Kijiji cha Kano katika Kata ya Natta.  

 Aidha, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Serengeti kumpatia ajira ya muda Mtaalamu wa TEHAMA Bwana Mathias Ngola Samwel ambaye anajitolea katika Halmashauri hiyo kuanzia mwaka 2021.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa