• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Hapi atangaza ratiba ya ziara ya Mheshimiwa Rais

Posted on: February 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo ametangaza rasmi ratiba ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan itakayofanyika katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 4 -7 Februari, 2022.

Mheshimiwa Hapi ametoa ratiba ya ziara ya Mheshimiwa Rais leo tarehe 1 Februari, 2022 katika mkutano na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mara uliofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Mheshimiwa Rais atapokelewa Bunda Mjini tarehe 4 Februari 2022 mchana baada ya hapo anatarajiwa kusalimiana na wananchi wa eneo la Kiabakari lililopo katika Wilaya ya Butiama” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa tarehe 5 Februari, 2022, Mheshimiwa Rais anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha maadhimisho ya miaka 45 ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo kitaifa yatafanyika katika Uwanja wa Karume, Manispaa ya Musoma.   

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, tarehe 6 Februari, 2022 Mheshimiwa Rais anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji wa Mgango- Kiabakari pamoja na kuwasalimia wananchi wa eneo la Mgango lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Aidha siku hiyo Mheshimiwa Rais anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) iliyopo katika Manispaa ya Musoma na kuzungumza na wananchi wa eneo la Kwangwa.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa tarehe 7 Februari, 2022 Mheshimiwa Rais anatarajiwa kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Wilayani Butiama na baadaye kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa chujio la maji, katika Mradi wa Maji wa Bunda, liliopo katika eneo la Nyabehu, Wilaya ya Bunda.

Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa Mheshimiwa Rais anatarajiwa kuhitimisha ziara yake kwa kuzungumza na wananchi wa Mji wa Bunda katika mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya sabasaba.   

Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi katika maeneo ambayo Mheshimiwa Rais atakapopita, maeneo atakayosalimiana na wananchi na atakapofanya mikutano ya hadhara na kumshangilia.

Aidha Mheshimiwa Hapi amewaalika Watanzania wote kujitokeza kwa wingi katika Maadhimisho ya Miaka 45 ya CCM ambapo Mkoa wa Mara umepewa heshima wa kuwa mwenyeji wa tukio hilo la kihistoria kwa Chama cha Mapinduzi.  

 Hii ni ziara ya kwanza ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tangu alivyoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Machi 2020.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa