• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

Posted on: May 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepokea taarifa za maandalizi ya mbio za mwenge wa uhuru kutoka Wilaya na Halmashauri za Mkoa wa Mara na kuzitaka Wilaya kuongeza nguvu katika maandalizi yam bio za mwenge za mwaka 2025.

“Angalieni mapungufu ya mwaka jana muone ni maeneo gani yanahitaji kurekebishwa kwa haraka kwa kuzingatia vigezo vya mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu” amesema Mhe. Mtambi

Mhe. Mtambi amewatahadhalisha kuwa bila maandalizi ya kutosha, Mkoa utapata aibu na kuwahakikishia kuwa uongozi wa Mkoa hautakubali kuaibika na kuwataka Wakuu wa Wilaya kuzisimamia Halmashauri kikamilifu.

Mhe. Mtambi amewataka Wakuu wa Wilaya na Kamati za Usalama za Wilaya kutembelea miradi iliyoainishwa na Halmashauri mapema ili kutoa nafasi za maandalizi kukamilika katika miradi itakayokubaliwa.

Mhe. Mtambi ameipongeza Wilaya ya Butiama kwa kuanza kufanya vikao vya maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru na kukagua miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 na kuipongeza taarifa ya maandalizi na mipango ya Wilaya ya Serengeti iliyowasilishwa katika kikao hicho.

Mhe. Mtambi ameitaka Wilaya ya Musoma kuboresha shughuli za hamasa ya mwenge wa uhuru kwa mwaka 2025 na kumtaka Katibu Tawala wa Mkoa kuitumia Brass Band ya SENAPA katika mapokezi na makabidhiano ya Mwenge na kumshirikisha Mhe. Julius Masubo Kambarage katika maandalizi ya mbio za mwege wa uhuru katika Mkoa wa Mara.  

Kwa upande wake, Mratibu wa Mbio za Mwenge Mkoa wa Mara Bwana Fidel Baragaye ameeleza kuwa kwa mwaka huu mbio za mwenge zitaingia katika Mkoa wa Mara tarehe 15 Agosti, 2025 kutokea Mkoa wa Simiyu na kukimbizwa katika Halmashauri zote tisa na kukabidhiwa Mkoa wa Mwanza tarehe 24 Agosti, 2025 katika Wilaya ya Ukerewe.

Bwana Baragaye amesema kwa mwaka 2025, Mwenge wa Uhuru hautapitia miradi iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru, ukaguzi wa miradi utakwenda sambamba na ukaguzi wa miundombinu ya zamani, mwenge utakagua kisayansi kwa kutumia vifaa vya kisasa na mwenge utaenda katika maeneo ambayo hayajapitiwa na Mwenge wa Uhuru.

Bwana Baragaye amesema ujumbe wa mbio za mwenge kwa mwaka 2025 inahusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ukiwa na kauli mbiu “Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 Amani na Utulivu”.

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizinduliwa tarehe 02 Aprili, 2025 katika Mkoa wa Pwani na kilele cha Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Wiki ya Vijana Kitaifa tarehe 14 Oktoba, 2025 katika Mkoa wa Mbeya.

Katika kikao hicho, Halmashauri zote za Mkoa wa Mara zimewasilisha taarifa kuhusu maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja na mikakati ya kuboresha katika mwaka 2025

Kikao cha tathmini ya mbio za mwenge mwaka 2024 na maandalizi ya mbio za mwenge 2025 kimehudhuriwa na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Menejimenti ya Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Waratibu wa Mbio za Mwenge wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa