• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Azitaka Halmashauri kubuni vyanzo vya mapato

Posted on: January 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Mara kubuni vyanzo vipya na endelevu vya mapato ili kuweza kuboresha makusanyo ya Halmashauri hizo na huduma kwa wananchi.

Akizungumza leo katika kikao cha tathmini ya utendaji kazi Mkoa wa Mara kilichofanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji, Mhe. Mtanda amezipongeza Halmashauri zilizofanya vizuri katika makusanyo ya robo ya kwanza na robo ya pili ya mwaka wa Fedha 2023/2024.

“Bila kuwa na mapato ya kutosha na endelevu, Halmashauri hazitaweza kutekeleza majukumu yake na hivyo kushindwa kujiendesha katika masuala ya msingi ya kuwahudumia wananchi kutokana na ukosefu wa fedha” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amezitaka Halmashauri kuacha kutegemea vyanzo vya mapato ambavyo havina tija tena kama vile uvuvi na kilimo ambavyo kwa muda mrefu vimekuwa havifanyi vizuri lakini ndio vyanzo vikuu vya mapato kwa baadhi ya Halmashauri.

Mhe. Mtanda amezishauri Halmashauri kuwekeza katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ili kuwezesha wananchi kuzalisha samaki kwa wingi na hivyo kuongeza samaki katika Ziwa Victoria na hatimaye kuongeza mapato ya Halmashauri.  

Amewataka Wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri kutoa msukumo zaidi katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kuwataka Maafisa Mipango wa Halmashauri kufanya ushirikishaji wa kutosha katika kubuni mipango ya Halmashauri zao.

Mhe. Mtanda amezitaka Halmashauri kuwafuatilia kwa ukaribu wakusanya mapato na kuhakikisha kuwa wanakusanya kupitia mfumo na wanaweka fedha benki kwa wakati kwa mujibu wa makubaliano ya mikataba yao.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashauri zote kuhakikisha kuwa watoto wote  waliopaswa kuanza darasa la awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza wanaenda shule na kuanza masomo kabla ya tarehe 31 Marchi, 2024.

Amewataka Wakuu wa Divisheni za Elimu kwa kushirikiana na viongozi na watendaji mbalimbali kufanya msako wa nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha watoto wote wanaenda shule kuanza masomo yao kwa mwaka 2024.

Awali akitoa taarifa ya uandikishaji, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Bulenga Makwasa amesema kwa sasa masomo yameshaanza japokuwa muda wa kupokea watoto bado upo hadi tarehe 31 Machi, 2024.

 Bwana Makwasa amewaomba viongozi kushirikiana ili kuwawezesha watoto wengi zaidi kuanza masomo na kunufaika na elimu bure inayotolewa kuanzia madarasa ya awali hadi Kidato cha Sita hapa nchini.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa