• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC azipongeza NGOs Mara

Posted on: September 20th, 2022

Mkutano Mkuu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Mara umefanyika leo katika ukumbi wa Uwekezaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kufunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee.

Akifungua mkutano huo, Mheshimiwa Mzee ameyapongeza mashirika yasiyo ya kiserikali Mkoa wa Mara kwa kutoa huduma mbalimbali kwa jamii ambazo zinawasaidia wananchi na kuwakwamua kwenye baadhi ya changamoto zinazowakabili.

“Napenda kuwapongeza kwa namna mnavyoshirikiana na Mkoa katika kutoa huduma mbalimbali kwa jamii ikiwa ni pamoja na kutoa elimu, miundombinu, msaada wa kisheria, utunzaji wa mazingira na kadhalika, hii inachochea maendeleo ya Mkoa wetu” alisema Mheshimiwa Mzee.

Hata hivyo Mheshimiwa Mzee ameyataka mashirika hayo katika utendaji wao kuacha alama katika maeneo wanayofanyia kazi ili hata miradi yao inapokuwa imeisha muda wake, jamii iwe na kumbukumbu nzuri ya miradi hiyo.

Aidha, Mheshimiwa Mzee ameyataka mashirika hayo kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa usajili wao na kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za utekelezaji wa majukumu kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara kupitia Msajili wa Mashirika yasiyo ya kiserikali.

Kwa upande wake, Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Mara Bibi Neema Ibamba ameeleza kuwa lengo la mkutano huo ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu uratibu na usimamizi wa Mashirika Yasiyo ya Kisherikali katika maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Bibi Ibamba ameeleza kuwa Mkoa wa Mara unajumla ya mashirika 286 yasiyo ya kiserikali lakini katika hayo mashirika 156 yapo hai lakini mashirika 130 hayapo hai na yanatarajiwa kufutwa kutokana na kutotmiza masharti na vigezo hususan kutokulipa ada.

“Ninaomba kuwasisitiza tutimize wajibu wetu ikiwa ni pamoja na kulipa ada, kutoa taarifa za utekelezaji wa majukumu na bajeti kwa mujibu wa sheria na taratibu za usajili” alisema Bibi Ibamba.

Bibi Ibamba ameyataka mashirika yaliyo katika orodha ya kufutwa, kufuata sheria na taratibu kwa kushirikiana na wasajili wasaidizi wa Mkoa na Halmashauri ili mashirika hayo yaweze kurudishiwa usajili na kuendelea na majukumu yao.

Aidha, Bibi Ibamba amewahamasisha wadau wote kujisajili kupitia http://register.jamii.go.tz ili kuweza kushiriki katika mkutano wa kitaifa wa mashirika yasiyo ya kiserikali utakaofanyika Dodoma tarehe 03-04 Oktoba, 2022.

Mkutano huo pia umehudhuriwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu na viongozi wa Kampeni ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Mkoa wa Mara ambao walitumia fursa hiyo kujitambulisha kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Mkoa wa Mara.

 Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi na wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali ya Mkoa wa Mara, Maafisa Maendeleo ya Jamii ambao ni Wasajili Wasaidizi wa Mashirika hayo ngazi za Halmashauri na Mkoa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa